" EWURA YANG’ARA SHIMMUTA, YAICHARAZA VIBAYA NEMC

EWURA YANG’ARA SHIMMUTA, YAICHARAZA VIBAYA NEMC

Pichani: Washambuliaji wa Timu ya EWURA (wenye jezi za bluu) wakishambulia timu pinzani wakati wa mchezo huo leo.

MOROGORO.

 Timu ya Mpira wa Wavu kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA) imeendelea kung’ara katika mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMMUTA) baada ya kuichakaza timu ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kwa seti mbili mfululizo.

Katika mchezo huo uliochezwa leo mkoani Morogoro, EWURA ilipata pointi 25 katika seti zote mbili, huku NEMC ikijitahidi lakini ikibaki na pointi 23 kwenye seti ya kwanza na 17 katika seti ya pili.

Mchezo huo uliovuta hisia za mashabiki ulitawaliwa na kasi, nidhamu na uchezaji wa kimkakati kutoka kwa EWURA, ambao washambuliaji wao walionekana kuwa imara zaidi dhidi ya ngome ya NEMC.

Pichani: Washambuliaji wa Timu ya EWURA (wenye jezi za bluu) wakishambulia timu pinzani wakati wa mchezo huo leo.

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment

Previous Post Next Post