Benki ya CRDB Bank Tawi la Geita imetoa
mafunzo kwa wateja wake wa taasisi mbalimbali kuhusu matumizi ya mfumo wa
Internet Benki, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kurahisisha huduma na kupunguza
msongamano wa wateja katika matawi.
Mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo wateja
ili waweze kufanya miamala yao nje ya tawi kwa urahisi, ikiwemo kufanya malipo
mbalimbali bila usumbufu.
Akifungua mafunzo hayo kwa niaba ya Mkuu wa
Wilaya ya Geita, Katibu Tawala wa Wilaya
hiyo, Lucy Beda, amesema kuwa matumizi ya Internet Benki yatawasaidia watumiaji
kuokoa muda na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao ya kifedha.
Kwa upande wake, Meneja wa Kanda wa benki hiyo,
Anselm Mwenda, amesema maboresho yaliyofanyika kwenye mfumo huo yameongeza
ufanisi mkubwa katika utumaji wa miamala, ambapo sasa mteja anaweza kutuma
fedha kwa watu wengi kwa wakati mmoja bila kukwama.
Ameeleza kuwa licha ya huduma hiyo kuwapo kwa
muda mrefu, bado baadhi ya wateja hawakuwa na uelewa wa kutosha kuhusu namna
bora ya kuitumia, hali iliyochochea benki hiyo kutoa mafunzo hayo.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wameeleza kufurahishwa na huduma ya Internet Benki, wakisema imewasaidia kuokoa muda na gharama, tofauti na awali ambapo walilazimika kubeba nyaraka mbalimbali kufika benki kwa ajili ya kufanya malipo, ikiwemo mishahara ya wafanyakazi.
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254
Post a Comment