" KIKAO CHA KAWAIDA CHA BARAZA LA WAZAZI MKOA WA SHINYANGA CHA KUFUNGA MWAKA 2025 CHAFANYIKA FEB 12,2026

KIKAO CHA KAWAIDA CHA BARAZA LA WAZAZI MKOA WA SHINYANGA CHA KUFUNGA MWAKA 2025 CHAFANYIKA FEB 12,2026


     Baraza la wazazi Mkoa wa Shinyanga limefanya kikao chake cha kawaida cha baraza la kufunga mwaka 2025 tarehe 12/02/2026, kikao hicho ambacho kilikuwa kinaongozwa na mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi Mkoa wa Shinyanga ndugu John Siagi.

 

Katika kikao hicho ndugu John Siagi amewaomba wajumbe wa Baraza kuwa na umoja na mshikamano wa dhati katika kuendeleza na kuimarisha jumuiya ya wazazi mkoa wa shinyanga, huku akiwapongeza wajumbe kwa ushirikiano wao katika utekelezaji wa majukumu ya chama kwa mwaka mzima wa 2025 ambapo mwenyekiti huyo ametumia nafasi hiyo kuwasalimia wajumbe na kuwatakia heri ya mwaka mpya 2026.

 

Ndugu John Siagi mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi mkoa wa Shinyanga ametumia wasaa kuzungumzia uchaguzi mkuu wa 2025, baraza la wazazi mkoa wa shinyanga linakipongeza chama cha mapinduzi kwa ushindi mkubwa katika ngazi zote za uongozi ikiwemo Udiwani wa Kata, Udiwani viti maalumu, Ubunge, Ubunge viti maalumu na Urais ambapo jumuiya ya wazazi mkoa wa Shinyanga limeeleza kuridhishwa na matokeo hayo na kuishukuru CCM kwa kuendelea kushika dola.

 

Ndugu Regina Ndulu katibu wa jumuiya ya wazazi mkoa shinyanga ameeleza kuwa jumuiya ya wazazi mkoa wa shinyanga inaendelea kuwa imara  na iko mstari wa mbele katika kutekeleza majukumu yake  ya chama kwa ufanisi na weledi, akisisitiza umuhimu wa kila mjumbe kutimiza wajibu wake ndani ya jumuiya na CCM kwa ujumla.

Ndugu Regina ameendelea kusisitiza wajumbe kuimarisha umoja na mshikamano, pamoja na kushiriki kikamilifu katika kazi za jumuiya ya wazazi na chama cha mapinduzi ili kuongeza ufasini wa utendaji kazi kwa uanachama wote waliopo kwenye nafasi mbalimbali za chama. Katika hatua nyingine jumuiya ya wazazi Mkoa wa Shinyanga  inatoa shukrani za dhati kwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, kwa kuibuka na ushindi wa kiti cha Urais katika uchaguzi mkuu wa 2025 na kutamka wazi kuwa “HONGERA SANA”

 

Kikao hicho cha baraza pia kimejadili kuimarisha uhai wa jumuiya ya wazazi, ambapo  Ndugu Regina Katibu wa wazazi mkoa wa Shinyanga amewahimiza wajumbe kuendelea kulipia ada za wanachama, kutoa hamasa  ya uandikishaji au usajili wa wanachama wapya na kuendelea kutoa elimu ngazi za matawi, mashina, kata, wilaya na mkoa ili kuongeza idadi ya wanachama kupitia jumuiya ya wazazi na chama cha mapinduzi kwa ujumla.

 

Aidha, jumuiya ya wazazi mkoa wa shinyanga imeeleza kuridhishwa na mafanikio ya kisiasa yaliyopatikana katika uchaguzi mkuu wa 2025, ambapo jumuiya ya wazazi imeweza kupata Madiwani wanao tokana na jumuiya ya wazazi wengi ambao sisi kama jumuiya ya wazazi mkoa wa Shinyanga ni mchango mkubwa sana kwa CCM na faraja kubwa  sana na hii ni kutokana na elimu, hamasa ya kuhamasisha wanachama kutia nia ya kugombea nafasi walizokuwa wanahitaji kuchukua fomu kwa ajili ya nafasi mbalimbali zilizokuwa zimetangazwa kama vile udiwani, ubunge na urais.

 

Ndugu, Edwin Peter Nyakanyenge mjumbe wa baraza kuu wazazi Taifa anayetokana na mkoa wa Shinyanga pia mjumbe wa kamati ya utekelezaji wazazi Taifa  ameshiriki kikamilifu baraza la funga mwaka 2025 mkoa wa Shinyanga kwa kuwahimiza wajumbe  wote wa baraza kwa nafasi zao kuwa wenye umoja na mshikamano wa dhati  katika kutekeleza majukumu ya kila mjumbe  na kwa nafasi yake aliyonayo kuhakikisha  jumuiya ya wazazi mkoa wa shinyanga inafanya kazi kwa ufanisi, weledi, upendo, amani, utulivu na mshikamano wa hali ya juu kuhakikisha jumuiya ya wazazi inasonga mbele bila kukwama au kukwamishwa na mtu asiye tekeleza  majukumu yake.

 

Ndugu Richard Masele  katibu wa itikadi na uenezi CCM Mkoa wa Shinyanga ameshiriki kwenye baraza la wazazi Mkoa wa Shinyanga kwa  niaba ya katibu wa CCM mkoa wa Shinyanga ndugu Odilia akisisitiza wajumbe wote wa baraza na wanachama kwa ujumla kila mjumbe kutambua majukumu yake na ametumia wasaa kuwakumbusha wajumbe kuwa na umoja na mshikamano   katika nafasi kwa kila mmoja aliyonayo aitumie kwa ufasaha na kwa weledi wa kuridhisha. Sambamba na hayo ndugu Richard Masele wamewasisitiza wajumbe wa baraza na wanachama kwa ujumla  kuendelea  kuvaa sale za chama bila woga.

 

Ndugu Jimotoli Jilala Maduka katibu wa Jumuiya ya wazazi CCM wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi leo tarehe 12/02/2026 asalimia baraza la wazazi mkoa wa Shinyanga kwa kuwashukuru na kuwapongeza viongozi wote wa jumuiya ya wazazi Mkoa wa Shinyanga na kuwatakia heri ya mwaka mpya 2026 ambapo  amewashukuru wajumbe wote kwa ujumla kupitia baraza hilo la funga mwaka 2025.

 

Kutokana na  baraza hili la jumuiya ya wazazi mkoa wa Shinyanga uongozi wa kamati ya utekelezaji wazazi mkoa wa Shinyanga umeshukuru kwa umoja na mshikamano, mchango, mawazo, ushauri pamoja na mambo mengine kwa kila mjumbe kwa kushiriki baraza hili la tarehe 12/02/2026.

 

Mwisho wa kikao, ndugu John Siagi  mwenyekiti wa jumuiya  ya wazazi mkoa wa Shinyanga amelifunga rasmi baraza la kufunga mwaka 2025 kwa kuwashukuru wajumbe wote kwa mawazo, mchango,maoni, mapendekezo, ushauri na kwa kuunga mkono juhudi, bidii pamoja na mipango na mikakati ya jumuiya hususani  katika utekelezaji wa miradi ya nyumba za watumishi wa jumuiya za wilaya na mkoa, miradi ya shule na masuala mengine yaliyojadiliwa katika kikao hicho cha baraza la tarehe 12/02/2026 na baada ya hapo mwenyekiti akafunga kikao mpaka siku nyingine.

Sambamba na hayo yote yaliyojadiliwa kwenye kikao jumuiya ya wazazi Mkoa wa Shinyanga kupitia baraza hilo la funga Mwaka imenufaika na mafunzo ya ufugaji wa Nguruwe.



  

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment

Previous Post Next Post