Na Mapuli Kitina Misalaba
Ziara ya Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)
Wilaya ya Shinyanga ya kukagua miradi ya maendeleo imeendelea, ambapo leo
kamati hiyo imetembelea mradi wa upanuzi wa mtandao wa majisafi unaotekelezwa
na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) katika Kata ya
Kolandoto.
Mradi huo unaotekelezwa kupitia fedha za Wizara ya
Maji kutoka Mfuko wa Maji wa Taifa, unahusisha upanuzi wa mtandao wa mabomba ya
majisafi katika kata za Kambarage, Ibadakuli, Kizumbi na Kolandoto ndani ya
Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga.
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mwenyekiti wa CCM
Wilaya ya Shinyanga mjini, Mhe. Anord Makombe, amesema chama kinaendelea
kufuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo ili kuhakikisha wananchi wanapata
huduma bora na fedha za serikali zinatumika kama ilivyokusudiwa.
Amesema mradi huo wa maji ni muhimu kwa wananchi kwani
utasaidia kupunguza changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama katika
maeneo mbalimbali ya manispaa hiyo.
Kwa upande wake, Meya wa Manispaa ya Shinyanga Mhe.
Salum Kitumbo amesema serikali ya Manispaa itaendelea kushirikiana na taasisi
mbalimbali kuhakikisha miradi ya maendeleo inatekelezwa kwa ufanisi na
kukamilika kwa wakati ili wananchi waweze kunufaika na huduma zinazotolewa.
Naye Katibu Tawala wa Wilaya ya Shinyanga Said Kitinga, aliyemwakilisha
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, amesema serikali inaendelea kusimamia miradi ya
maendeleo ili kuhakikisha inatekelezwa kwa viwango vinavyotakiwa na kukamilika
kwa wakati uliopangwa.
Amesema utekelezaji wa miradi hiyo una lengo la
kuboresha maisha ya wananchi kwa kuwapatia huduma muhimu kama maji safi na
salama karibu na maeneo yao ya makazi.
Kwa upande wao, baadhi ya wananchi wa eneo hilo wameipongeza
serikali kwa kuleta mradi huo wa majisafi huku wakiomba ukamilike kwa wakati
ili uweze kuondoa changamoto ya kutembea umbali mrefu kufuata maji.
Kwa mujibu wa taarifa ya SHUWASA, ambayo imesomwa na kaimu
Mkurugenzi mamlaka hiyo Mhandisi Uswege Musa, mradi wa uboreshaji wa huduma ya
majisafi katika Manispaa ya Shinyanga ulianza kutekelezwa mwezi Septemba 2025
na unatarajiwa kukamilika mwezi Machi 2026.
Mradi huo unahusisha upanuzi wa mtandao wa mabomba ya
maji kwa urefu wa kilomita 8.5 kwa gharama ya zaidi ya Shilingi milioni 119,
ambapo unatarajiwa kuwanufaisha takribani wananchi 2,850.
Katika Kata ya Kolandoto, mradi huo umebuniwa
kuhudumia maeneo ya Mwanubi na Mwamala, ambapo takribani wananchi 1,749
wanatarajiwa kunufaika na huduma ya maji safi na salama.
Kukamilika kwa mradi huo kunatarajiwa kupunguza
changamoto ya wananchi kutembea umbali mrefu kutafuta maji pamoja na kusaidia
kupunguza magonjwa yanayotokana na matumizi ya maji yasiyo salama.
kaimu Mkurugenzi mamlaka hiyo Mhandisi Uswege Musa, akizungumza baada ya kusoma taarifa ya mradi huo.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga, Makombe, akizungumza wakati wa ziara ya kukagua mradi wa maji unaotekelezwa na SHUWASA.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga, Makombe, akizungumza wakati wa ziara ya kukagua mradi wa maji unaotekelezwa na SHUWASA.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga, Makombe, akizungumza wakati wa ziara ya kukagua mradi wa maji unaotekelezwa na SHUWASA.
Meya wa Manispaa ya Shinyanga Salum Kitumbo akizungumza kuhusu umuhimu wa mradi wa maji unaotekelezwa na SHUWASA na faida zake kwa wananchi wa Kolandoto.
Samwel Jackson katibu wa mbunge wa jimbo la Shinyanga mjini akizungumza wakati wa kukagua mradi wa maji unaotekelezwa na SHUWASA.
Samwel Jackson katibu wa mbunge wa jimbo la Shinyanga mjini akizungumza wakati wa kukagua mradi wa maji unaotekelezwa na SHUWASA.

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254















Post a Comment