Na mwandishi wetu, Misalaba Media MbeyaMwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mbeya Mjini, Emmanuel Mwalupindi, amekabidhi zawadi ya jezi kwa timu iliyofanya vizuri na kuibuka washindi katika ligi ya wanawake mkoani Mbeya, ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha na kuendeleza michezo kwa wanawake.Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano hayo, Mwalupindi amesema kuwa michezo ni nyenzo muhimu ya kuwawezesha wanawake kijamii na kiuchumi, huku akisisitiza umuhimu wa kuendelea kuwekeza katika sekta hiyo ili kukuza vipaji vya vijana wa kike.Ameongeza kuwa Jumuiya ya Wazazi itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha wanawake wanapata fursa zaidi za kushiriki katika michezo na kuonesha uwezo wao, jambo litakalosaidia kuinua hadhi ya michezo ya wanawake katika ngazi ya mkoa na taifa kwa ujumla.Kwa upande wao, baadhi ya washindi wa ligi hiyo wameeleza kufurahishwa na zawadi hiyo, wakisema kuwa imewapa motisha ya kuendelea kufanya vizuri zaidi katika mashindano yajayo. Wameomba wadau wengine kujitokeza kusaidia maendeleo ya michezo ya wanawake ili kufikia mafanikio makubwa zaidi.Ligi hiyo ya wanawake mkoani Mbeya imekuwa chachu ya kugundua na kukuza vipaji vya soka kwa wanawake, huku ikitoa fursa kwa timu mbalimbali kushiriki na kujenga ushindani wenye tija.



SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment