" TAMASHA KUBWA LA MWANAMKE CHUMA 2026 KUFANYIKA APRILI 11 KAHAMA

TAMASHA KUBWA LA MWANAMKE CHUMA 2026 KUFANYIKA APRILI 11 KAHAMA


Kituo cha redio cha Gold FM, kimeendelea kujipambanua kama chachu ya maendeleo ya kijamii kwa kuhamasisha na kuinua nafasi ya mwanamke tangu kuanzishwa kwake mwaka 2021.

Kupitia maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, kituo hicho kimeendelea kufanya jukwaa maalum lijulikanalo kama “MWANAMKE CHUMA”, lenye lengo la kuhamasisha, kuimarisha na kuwawezesha wanawake kwa kuwapa nafasi ya kujifunza, kushirikiana, kuunganishwa na kutambulika katika jamii.

Mwaka huu, Tamasha la Mwanamke Chuma 2026 linatarajiwa kufanyika Jumamosi, Aprili 11, 2026 katika Ukumbi wa Malex Hall, Kahama, kuanzia saa 11 jioni, likiwa na kaulimbiu isemayo: “NGUVU YA UJASIRI”.

Tamasha hilo litapambwa na burudani kutoka kwa nguli wa muziki wa Taarab nchini, Mzee Yusuph, huku mtaalamu wa maendeleo ya familia na uchumi Dr. Chris Mauki akitoa elimu muhimu kwa wanawake na wanaume. Aidha, mshereheshaji wa tukio hilo anatarajiwa kuwa Dr. Kumbuka, ambaye ataleta hamasa na burudani ya kipekee jukwaani.

Mgeni rasmi katika tukio hilo anatarajiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, ambaye atahitimisha rasmi tamasha hilo kubwa linalokusanya watu kutoka maeneo mbalimbali hasa ya Kanda ya Ziwa.

Mbali na burudani na elimu, tamasha hilo pia litahusisha utoaji wa tuzo mbalimbali kwa wanawake waliofanya vizuri katika nyanja tofauti, ikiwemo ubunifu na ushonaji, saluni bora, mwanamke mwenye ushawishi, mjasiriamali bora na chipukizi, mpishi bora pamoja na kikundi bora.

Kwa mujibu wa waandaaji, tukio hilo linatarajiwa kuwa jukwaa muhimu la kuibua vipaji, kuhamasisha ujasiri na kuongeza mchango wa mwanamke katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

🎟️ Viingilio vya tamasha hilo ni:

  • Regular – 30,000/=
  • V.I.P – 50,000/=
  • Table – 500,000/=

📞 Kwa mawasiliano na nafasi za kuhifadhi tiketi: 0744 357 578

Wananchi wote wa Kahama, Kanda ya Ziwa na maeneo ya jirani wanahimizwa kujitokeza kwa wingi kushiriki tukio hili adhimu ambalo si tu burudani, bali pia ni jukwaa la kuamsha ndoto, kuthubutu na kuonesha nguvu ya mwanamke wa kisasa.

Usikose kuwa sehemu ya historia ya Mwanamke Chuma 2026 – huu si usiku wa kawaida, ni usiku wa kuamsha uthubutu na mafanikio!



 SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

 
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment

Previous Post Next Post