" CHINA YAMNYONGA MLANGUZI WA DAWA ZA KULEVYA KUTOKA UFARANSA

CHINA YAMNYONGA MLANGUZI WA DAWA ZA KULEVYA KUTOKA UFARANSA






Wizara ya Mambo ya Nje ya Ufaransa imetangaza kwamba Mfaransa mwenye umri wa miaka 62 ambaye alikuwa amehukumiwa kifo na China kwa ulanguzi wa dawa za kulevya amenyongwa.

Ufaransa imesema alipatikana na hatia ya ulanguzi wa dawa za kulevya mnamo 2010.

Serikali ya Ufaransa imesema kwamba mtu huyo alikuwa hapaswi kuhukumiwa kifo, kwamba badala yake angepewa msamaha lakini ombi hilo halikukubaliwa kamwe.

Wizara ya Mambo ya Nje ya Ufaransa ilisema Mawakili hawakuruhusiwa kumwakilisha katika kesi yake ya mwisho katika Mji wa Guangzhou, Kusini mwa China.

Kifungu cha 347 cha sheria ya jinai ya China kinasema kuwa usafirishaji, usambazaji na utengenezaji wa dawa za kulevya ni uhalifu mkubwa.

Ukipatikana na hatia, unaweza kuadhibiwa kulingana na ukubwa wa uhalifu, na makosa madogo yanapata adhabu nyepesi, wakati uhalifu mkubwa unaweza kuhukumiwa kifungo cha maisha au adhabu ya kifo.

Post a Comment

Previous Post Next Post