Na Mapuli Kitina Misalaba
Katibu wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Lukomanga Jinyage,
amewataka vijana wa vyuo mkoani humo kuthamini na kulinda amani ya nchi,
akisisitiza kuwa amani ndiyo msingi wa maendeleo ya taifa na ustawi wa vizazi
vijavyo.
Akizungumza na wanachuo wa Chuo cha St. Joseph mjini
Shinyanga wakati wa ziara ya Seneti katika vyuo mbalimbali, Jinyage amesema
hakuna mtu kutoka nje ya nchi atakayekuja kulinda amani ya Tanzania, hivyo ni
wajibu wa kila mwananchi hususan vijana kuhakikisha inalindwa na kudumishwa.
“Tambueni kuwa amani ya nchi yenu ni
hazina kubwa sana. Hakuna mtu kutoka nje atakayekuja kuitunza kwa niaba yenu,
hivyo ni jukumu letu sote kuhakikisha tunailinda kwa nguvu zote kwa manufaa ya
kizazi cha sasa na kijacho,” amesema Jinyage.
Ameonya kuwa baadhi ya kauli kutoka kwa watu katika
jamii, wakiwemo wazee, zinaweza kuwa chanzo cha kuvuruga amani endapo
hazitachukuliwa kwa busara, akiwataka vijana kuwa na uelewa mpana na kufanya
maamuzi sahihi.
“Wakati mwingine unaweza kusikia ushawishi
wa kushiriki vitendo vinavyoweza kuvuruga amani. Ni muhimu vijana mkatumia
busara na kujiuliza kama kweli yanayoshauriwa yana manufaa kwa taifa. Kila
mmoja ana wajibu wa kulinda amani,” ameongeza.
Aidha, amewasisitiza wanachuo kuwa mstari wa mbele
katika kuhamasisha mshikamano, kuheshimu sheria na kushiriki katika shughuli za
maendeleo ili kuhakikisha nchi inaendelea kuwa salama na yenye utulivu.
Ziara ya Seneti Mkoa wa Shinyanga inaendelea katika vyuo mbalimbali, ikiwa na lengo la kutoa elimu, kusikiliza changamoto za wanachuo na kuimarisha uongozi wa wanafunzi katika taasisi za elimu ya juu.
Viongozi wa Seneti Mkoa wa Shinyanga wakizungumza na wanachuo wa St. Joseph, wakitoa elimu kuhusu fursa za ajira, uongozi na masuala ya jamii.
Katibu wa Seneti Mkoa wa Shinyanga Lukomanga Jinyage akieleza umuhimu wa kulinda amani na mshikamano kwa maendeleo ya vijana na taifa kwa ujumla.
Katibu Hamasa wa Seneti Mkoa wa Shinyanga Sharon Callist Mathias akihamasisha wanachuo kushiriki kikamilifu katika uongozi na shughuli za maendeleo.

Katibu Hamasa wa Seneti Mkoa wa Shinyanga Sharon Callist Mathias akihamasisha wanachuo kushiriki kikamilifu katika uongozi na shughuli za maendeleo.

Katibu wa Seneti Wilaya ya Shinyanga Mjini, Samwel Samson akizungumza na wanachuo, akisisitiza nidhamu, bidii katika masomo na kujiepusha na makundi yasiyofaa.


Wanachuo wa St. Joseph wakifuatilia kwa makini hotuba za viongozi wa Seneti Mkoa wa Shinyanga leo Aprili 22, 2026.

Wanachuo wa St. Joseph wakifuatilia kwa makini hotuba za viongozi wa Seneti Mkoa wa Shinyanga leo Aprili 22, 2026.

Wanachuo wa St. Joseph wakifuatilia kwa makini hotuba za viongozi wa Seneti Mkoa wa Shinyanga leo Aprili 22, 2026.
Viongozi wa Seneti Mkoa wa Shinyanga wakiwa katika kikao na Makamu Mkuu wa Chuo cha St. Joseph Kampasi ya Shinyanga, wakijadili maendeleo ya wanachuo na ushirikiano wa taasisi.
Viongozi wa Seneti wakifanya mazungumzo na Makamu Mkuu wa Chuo cha St. Joseph kuhusu fursa na changamoto zinazowakabili wanachuo.
Picha ya pamoja baada ya mazungumzo.
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254
















Post a Comment