" MWENYEKITI CCM MPANDA ASIKILIZA KERO ZA WANANCHI TULIENI, ASISITIZA UMOJA NA HAKI

MWENYEKITI CCM MPANDA ASIKILIZA KERO ZA WANANCHI TULIENI, ASISITIZA UMOJA NA HAKI


Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Mpanda, Joseph Lwamba, amefanya ziara katika Mtaa wa Tulieni, Kata ya Nsemulwa, Manispaa ya Mpanda Aprili 17, 2026 kwa lengo la kusikiliza, kupokea na kutatua kero za wananchi.

Katika ziara hiyo, Lwamba alikutana na wakazi wa eneo hilo na kuwapa nafasi ya kueleza changamoto mbalimbali zinazowakabili, huku akiahidi kuzifanyia kazi kwa kushirikiana na viongozi wa ngazi husika.

Akizungumza na wananchi, alisisitiza umuhimu wa umoja na mshikamano katika kujiletea maendeleo, akibainisha kuwa ushirikiano kati ya wananchi na viongozi ni msingi wa kutatua changamoto za jamii.

Aidha, alitoa wito kwa wananchi kuwa makini katika masuala ya ununuzi na uuzaji wa viwanja ili kuepuka migogoro ya ardhi, huku akiwataka viongozi wa mtaa kusimamia kikamilifu majukumu yao kwa uadilifu na uwajibikaji.

Lwamba pia aliwahimiza wananchi kuendeleza upendo na amani, pamoja na kuacha woga katika kutetea haki zao kwa kufuata taratibu na sheria zilizopo.

Katika hatua nyingine, alisisitiza umuhimu wa kupunguza migogoro ya ardhi katika Mtaa wa Tulieni kwa kushirikiana na mamlaka husika, huku akihimiza uwajibikaji kwa kila mmoja katika kulinda na kusimamia rasilimali za maeneo yao.

Ziara hiyo ni sehemu ya juhudi za viongozi wa chama kusogea karibu na wananchi ili kusikiliza na kutatua changamoto zao kwa wakati.

Ndg. Joseph Lwamba, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mpanda na mjumbe wa Kamati ya Siasa wilaya, akisikiliza kero za wananchi wa Mtaa wa Tulieni, Kata ya Nsemulwa, Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda.Ndg. Jimotoli Jilala Maduka, Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Mpanda na akimwakilisha Katibu wa CCM Wilaya ya Mpanda, Ndg. Musa Ramadhan Mwevi, akishiriki kikamilifu katika mkutano wa hadhara wa kusikiliza kero za wananchi uliofanyika Mtaa wa Tulieni, Kata ya Nsemulwa, Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda.

SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

 

Post a Comment

Previous Post Next Post