Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga limefanikiwa
kukamata jumla ya watuhumiwa 35 wanaodaiwa kujihusisha na vitendo vya uhalifu
katika operesheni zilizofanyika kuanzia Machi 1 hadi Machi 31, 2026.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP), kukamatwa kwa watuhumiwa hao kunahusishwa na operesheni maalum zilizofanyika katika maeneo ya mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa ya SGR katika wilaya za Msalala na Shinyanga.
Katika operesheni hizo, Polisi wamefanikiwa kukamata
vielelezo mbalimbali vikiwemo pinde 306, nondo, mabomba 32 ya ukubwa wa mm12,
stendi za makarasha 12 pamoja na mabomba ya mraba (square pipe) 65.
Aidha, kwa upande wa usalama barabarani, Jeshi la
Polisi kupitia Kikosi cha Usalama Barabarani limeendesha operesheni dhidi ya
madereva wanaokiuka sheria, ambapo madereva wawili walifungiwa leseni zao kwa
kipindi cha miezi mitatu baada ya kubainika kuendesha gari kwa mwendo kasi
zaidi ya kilomita 80 kwa saa (80KPH).
Katika ukaguzi huo, jumla ya makosa 5,648 ya
barabarani yalibainika, ambapo makosa ya magari yalikuwa 4,044 na yale ya
bajaji na pikipiki yalifikia 1,604, huku wahusika wakitozwa faini papo kwa
papo.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga linatoa wito kwa
wananchi kuendelea kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama kwa kutoa
taarifa za uhalifu, sambamba na kuwakumbusha wazazi na walezi kuongeza
uangalizi kwa watoto katika kipindi hiki cha Sikukuu za Pasaka.
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment