Na Mapuli Kitina Misalaba
Baadhi ya wakazi wa Manispaa ya Shinyanga
wamezungumzia umuhimu wa kudumisha amani katika maisha ya kila siku, wakisema
kuwa amani ni msingi wa maendeleo ya mtu mmoja mmoja na jamii kwa ujumla.
Akizungumza na Misalaba Media, Mkazi wa Mtaa wa Miti
Mirefu, Kata ya Mjini, Mzee Ndulu Mipawa amesema kuwa bila amani hakuna
shughuli za maendeleo zinazoweza kufanyika kwa ufanisi, akiwahimiza wananchi
kuendelea kulinda utulivu uliopo.
Kwa upande wake, Mkazi wa Kata ya Kitangili, Bwana
Philipo Maganga Machiya, amesema kuwa amani huleta mshikamano miongoni mwa watu
na kusaidia kujenga mahusiano mazuri ndani ya jamii, hali inayochochea
maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Naye Rebeka Godfury, mkazi wa Kata ya Mjini, ameeleza
kuwa amani inapaswa kuanzia ngazi ya familia, akisisitiza kuwa maadili mema na
kuheshimiana ni nguzo muhimu katika kuimarisha utulivu wa jamii.
Aidha, Mkazi wa Nguzonane, Farda Ntauma, amesema kuwa
vijana wanapaswa kuelimishwa juu ya umuhimu wa amani ili kuepuka vitendo
vinavyoweza kuhatarisha usalama, akiongeza kuwa jamii yenye amani huwavutia
wawekezaji na kuongeza fursa za ajira.
Kwa pamoja, wananchi hao wamewataka Watanzania kuendelea kudumisha mshikamano, kuheshimu sheria na mamlaka zilizopo ili kuhakikisha amani inaendelea kuwepo na kuwa chachu ya maendeleo endelevu.

Mzee Ndulu Mipawa

Bwana Philipo Maganga Machiya

Rebeka Godfury
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254
Post a Comment