" HOME BOYS YAIONDOA MANHEIGANA NIACHEKONA CUP 2026

HOME BOYS YAIONDOA MANHEIGANA NIACHEKONA CUP 2026


Na Mapuli Kitina Misalaba


Mzunguko wa pili wa marudiano wa mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 umeanza rasmi leo Jumatano Mei 27, 2026 kwa mchezo wa ushindani mkubwa uliochezwa katika uwanja wa Mwabenda kata ya Solwa, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga ambapo timu ya HOME BOYS imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya MANHEIGANA FC.

Kutokana na matokeo hayo, timu ya MANHEIGANA FC imeondolewa rasmi kwenye mashindano hayo baada ya kupoteza pointi muhimu katika mchezo wa leo.

Ikumbukwe kuwa timu hizo mbili ndiyo zilizofungua rasmi mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 ambapo katika mchezo wa ufunguzi zilitoshana nguvu kwa sare ya bao 1-1 kabla ya HOME BOYS kuibuka na ushindi katika mchezo wa leo wa marudiano.

Mashabiki wa HOME BOYS wameendelea kuonesha furaha na matumaini makubwa kufuatia ujio wa kocha mpya wa timu hiyo baada ya kuachana na kocha wa awali, huku wakiamini mabadiliko hayo yataisaidia timu yao kufanya vizuri zaidi katika mashindano hayo.

Akizungumza baada ya ushindi huo, kocha mpya wa HOME BOYS amesema malengo yake makubwa ni kuhakikisha timu hiyo inafika hatua ya fainali na hatimaye kutwaa ubingwa wa NIACHEKONA CUP 2026.

Kwa upande wao viongozi wa MANHEIGANA FC wamemshukuru mwandaaji wa mashindano hayo Bwana Paul Daud Augustino kwa kuwapa nafasi ya kushiriki katika mashindano hayo huku wakisema wamejifunza mambo mengi kupitia ushindani walioupata ndani ya ligi hiyo.

Aidha baada ya kuondolewa katika mashindano hayo, timu hiyo imeomba kupewa nafasi ya Mshindwa bora (Best Rooza) kutokana na namna walivyopambana na kushiriki kwa ushindani katika michezo yao yote.

Baada ya mchezo huo, Katibu wa Kamati ya Mashindano Sambayi Jilya ametangaza ratiba ya mchezo wa kesho ambapo timu ya MWASENGE FC kutoka kata ya Salawe itamenyana na UFUKUNYUNGU FC kutoka kata ya Ngokolo mjini Shinyanga katika mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.

Sambayi ameendelea kuwahimiza wananchi pamoja na mashabiki wa timu hizo kujitokeza kwa wingi katika uwanja wa Mwabenda kushuhudia burudani ya soka pamoja na vipaji vya vijana vinavyoendelea kuonekana kupitia mashindano hayo.

Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yameandaliwa na Bwana Paul Daud Augustino kupitia ufadhili wa shirika la Lushu Foundation kwa lengo la kuibua vipaji vya vijana, kukuza michezo pamoja na kuimarisha mshikamano wa jamii kupitia soka.

Kwa huduma za ushereheshaji wa shughuli mbalimbali, matangazo pamoja na burudani unaweza kuwasiliana na MC NIACHEKONA kupitia namba 0757 267 738.

Timu ya MANHEIGANA FC.


 SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment

Previous Post Next Post