" WAWILI WAHUKUMIWA JELA KWA KUSAMBAZA TAARIFA ZA UONGO

WAWILI WAHUKUMIWA JELA KWA KUSAMBAZA TAARIFA ZA UONGO

Na Mapuli Kitina Misalaba

Wakazi wawili wa Manispaa ya Kahama mkoani Shinyanga wamehukumiwa vifungo vya jela baada ya kupatikana na hatia ya kusambaza taarifa za uongo zilizozua taharuki katika jamii.

Akizungumza na vyombo vya habari leo Aprili 9, 2026, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, SACP Janeth Magomi, amewataja waliohukumiwa kuwa ni Kisaka Elininhaki (22), mfanyabiashara, na Makoye James (20), dereva.

Kwa mujibu wa Kamanda Magomi, wawili hao walikamatwa kufuatia kusambaza taarifa zisizo za kweli wakidai kupotea kwa sehemu nyeti kimujiza baada ya kuguswa, hali iliyosababisha hofu na taharuki kwa wananchi.

Ameeleza kuwa baada ya kufikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kahama, walipatikana na hatia ya kusambaza taarifa za uongo.

Katika hukumu hiyo, Kisaka Elininhaki amehukumiwa kifungo cha miezi sita jela, huku Makoye James akihukumiwa kifungo cha miezi mitano jela.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga limewakumbusha wananchi kuwa kusambaza taarifa za uongo ni kosa la jinai linaloweza kusababisha madhara makubwa kwa jamii, likiwemo uvunjifu wa amani.

Aidha, wananchi wametakiwa kutoa taarifa sahihi na kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama ili kudumisha amani na utulivu.

 SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

 
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment

Previous Post Next Post