Na Mapuli Kitina Misalaba
Baadhi ya wadau wa michezo katika kata ya Solwa,
Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga wamepongeza mashindano ya NIACHEKONA CUP
2026 wakisema yamekuwa na mchango mkubwa katika kuimarisha afya ya akili na
mwili kwa vijana pamoja na wananchi wanaofuatilia michezo hiyo.
Wakizungumza na Misalaba Media, wadau hao wamesema
michezo ni nyenzo muhimu ya kujenga afya bora, kuimarisha mshikamano wa jamii
na kuwasaidia vijana kutumia muda wao katika shughuli zenye manufaa.
Wamempongeza mwandaaji wa mashindano hayo, Bwana Paul
Daud Augustino maarufu MC NIACHEKONA, kwa juhudi zake za kuendeleza michezo na
kuibua vipaji vya vijana kupitia mashindano hayo yanayoendelea katika uwanja wa
Mwabenda.
Aidha, wamemshauri kuangalia uwezekano wa kuanzisha
timu au programu ya mbio za jogging ili kuwapa wananchi na vijana fursa zaidi
za kushiriki shughuli za mazoezi na kuimarisha afya zao.
Wadau hao pia wamewaomba wadau wengine wa maendeleo,
wafadhili na wadau wa michezo kuendelea kumuunga mkono MC NIACHEKONA ili vijana
wengi zaidi waweze kunufaika na michezo kama sehemu ya ajira, ukuzaji wa vipaji
na maendeleo ya kijamii.
Sambamba na hilo, wamewahimiza wafanyabiashara na
wajasiriamali kutumia fursa ya mashindano hayo kwa kufika katika uwanja wa
Mwabenda wakati wa mechi zinazoendelea kila siku jioni ili kuuza bidhaa na
huduma mbalimbali, hatua ambayo inaweza kuongeza kipato chao na kuchangia
ukuaji wa uchumi wa eneo hilo.
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment