" SONGAMBELE MHANGU YATINGA HATUA INAYOFUATA KWA KISHINDO BAADA YA KUIFUNGA SHILIMA FC MABAO 4-0

SONGAMBELE MHANGU YATINGA HATUA INAYOFUATA KWA KISHINDO BAADA YA KUIFUNGA SHILIMA FC MABAO 4-0


Na Mapuli Kitina Misalaba

Timu ya SONGAMBELE MHANGU kutoka kata ya Salawe imeendelea kuonesha ubora wake katika mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya SHILIMA FC kutoka Mkoa wa Mwanza katika mchezo wa marudiano uliochezwa kwenye uwanja wa Mwabenda kata ya Solwa, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.

Ushindi huo umeihakikishia SONGAMBELE MHANGU tiketi ya kusonga mbele katika hatua inayofuata ya mashindano hayo huku safari ya SHILIMA FC ikifikia tamati rasmi.

Ikumbukwe kuwa katika mchezo wa kwanza uliochezwa kati ya timu hizo, SONGAMBELE MHANGU iliibuka na ushindi wa bao 1-0, hivyo kufikisha jumla ya mabao 5-0 katika michezo yote miwili ya hatua ya mtoano.

Kutokana na ushindi huo, SONGAMBELE MHANGU sasa itakutana na DUARA FC katika hatua inayofuata ya mashindano hayo baada ya DUARA FC kufuzu jana dhidi ya MWANDUTU FC.

Baada ya mchezo huo, Katibu wa Kamati ya Mashindano Sambayi Jilya ametangaza ratiba ya mchezo wa kesho ambapo NZOZA FC itamenyana na NYUNDO FC katika pambano linalotarajiwa kuvuta hisia za mashabiki wengi wa soka ndani na nje ya kata ya Solwa.

Sambayi amewahimiza wananchi, wadau wa michezo pamoja na mashabiki wa timu hizo kujitokeza kwa wingi katika uwanja wa Mwabenda ili kuendelea kushuhudia michezo yenye ushindani mkubwa na vipaji vinavyochipukia kupitia mashindano hayo.

Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yameandaliwa na Bwana Paul Daud Augustino maarufu MC NIACHEKONA kupitia ufadhili wa shirika la Lushu Foundation yakiwa na lengo la kuibua vipaji vya vijana, kukuza michezo, kuimarisha amani na kuleta mshikamano katika jamii.

Kwa huduma za ushereheshaji wa shughuli mbalimbali, matangazo na matukio ya kijamii, MC NIACHEKONA anapatikana kupitia namba 0757 267 738.

Kikosi cha Songambele Mhangu FC.

Post a Comment

Previous Post Next Post