Na Mapuli Kitina Misalaba
Baadhi ya wananchi wa kata ya Solwa na maeneo jirani
wamezungumzia umuhimu wa michezo katika jamii wakisema imeendelea kuwa nyenzo
muhimu ya kuimarisha afya, amani, mshikamano pamoja na maendeleo ya vijana.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika uwanja wa
Mwabenda, wananchi hao wamesema michezo imekuwa ikiwakutanisha watu kutoka
maeneo mbalimbali na kuwapa nafasi ya kubadilishana uzoefu, kujenga urafiki na
kuimarisha mahusiano miongoni mwao.
Wameeleza kuwa vijana wengi wanaposhiriki michezo au
kufuatilia mashindano mbalimbali hupata fursa ya kutumia muda wao katika
shughuli zenye manufaa badala ya kujihusisha na vitendo vinavyoweza kuhatarisha
mustakabali wao na maendeleo ya jamii.
Aidha wamesema michezo ni sehemu ya ajira na uchumi
kwani huwasaidia wafanyabiashara, waendesha bodaboda, mama lishe na makundi
mengine ya kijamii kupata kipato kupitia mikusanyiko ya watu wanaofika
kushiriki au kushuhudia michezo.
Wananchi hao pia wamepongeza mashindano ya NIACHEKONA
CUP 2026 yanayoendelea katika uwanja wa Mwabenda kwa kuendelea kutoa nafasi kwa
vijana kuonesha vipaji vyao huku yakihamasisha amani, umoja na mshikamano
katika jamii.
Wamempongeza mwandaaji wa mashindano hayo, Bwana Paul
Daud Augustino maarufu MC NIACHEKONA kwa juhudi zake za kuendeleza michezo
katika eneo hilo na kuwapa vijana jukwaa la kuonesha uwezo wao.
Wamewataka wadau mbalimbali wa michezo kuendelea
kuunga mkono mashindano hayo ili yaweze kukua zaidi na kuwafikia vijana wengi
wanaohitaji fursa za kuonesha vipaji vyao.
Hadi sasa baadhi ya timu zilizofanikiwa kutinga hatua
inayofuata ya mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 ni pamoja na HOME BOYS,
WAFUKUNYUNGU FC, DUARA FC na SONGAMBELE MHANGU huku timu nyingine zikiendelea
kupambana kutafuta nafasi ya kuungana nazo katika hatua inayofuata ya
mashindano hayo.
Kwa huduma za ushereheshaji wa shughuli mbalimbali, matangazo na matukio ya kijamii, MC NIACHEKONA anapatikana kupitia namba 0757 267 738.

SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254





Post a Comment