Na Mapuli Kitina Misalaba
Ziara ya viongozi wa Seneti ya Vyuo na Vyuo Vikuu Mkoa
wa Shinyanga imeendelea leo kwa kutembelea Chuo cha Serikali za Mitaa kilichopo
mjini Shinyanga pamoja na Chuo cha Ualimu SHYCOM, ambapo viongozi hao wametoa
elimu mbalimbali kwa wanachuo kuhusu uongozi, uzalendo, fursa za maendeleo na
wajibu wa vijana katika jamii.
Viongozi ambao wameshiriki katika ziara hiyo ni
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga Jackson Aloyce Mwizarubi, Katibu wa
Seneti Mkoa wa Shinyanga Lukomanga Jinyage Jiboli pamoja na Katibu Hamasa wa
Seneti, Sharon Callist Mathias.
Akizungumza na wanachuo hao, Mwenyekiti wa Seneti Mkoa
wa Shinyanga Jackson Aloyce Mwizarubi, amewataka vijana kutumia vizuri muda wao
wa masomo kwa kujijenga kitaaluma na kiuongozi ili waweze kuwa sehemu ya
maendeleo ya taifa.
“Nyinyi ndiyo nguvu ya taifa la kesho.
Tumia vizuri nafasi mliyoipata ya elimu, jengeni nidhamu, muwe wabunifu na
msiogope kutumia ujuzi wenu kujitengenezea ajira,”
amesema Mwizarubi.
Kwa upande wake, Katibu wa Seneti Mkoa wa Shinyanga
Lukomanga Jinyage Jiboli, amesisitiza umuhimu wa amani, mshikamano na uzalendo
kwa vijana wa vyuo, akiwataka kuwa mfano bora katika jamii.
“Amani ya nchi yetu ni msingi wa maendeleo
yetu. Vijana tunapaswa kuwa mstari wa mbele kuilinda na kuhakikisha tunaishi
kwa upendo, mshikamano na kuheshimu taratibu zilizopo,”
amesema Jiboli.
Naye Katibu Hamasa wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Sharon
Callist Mathias, amewahamasisha wanachuo kujiamini, kushiriki katika shughuli
za maendeleo pamoja na kutumia vyema fursa zinazopatikana kupitia elimu na
uongozi.
“Msikubali kurudishwa nyuma na changamoto.
Chuo ni sehemu ya kujifunza maisha, kujenga uwezo na kujiandaa na mustakabali
wenu. Changamkieni fursa zinazowazunguka,” amesema Sharon.
Baadhi ya wanachuo waliohudhuria mikutano hiyo
wamewashukuru viongozi wa Seneti kwa kuwafikia na kutoa elimu yenye manufaa kwa
vijana, huku wakiahidi kuwa wazalendo, kuzingatia masomo yao na kutumia fursa
mbalimbali zinazotolewa kupitia Seneti.
Aidha, viongozi hao wamewahimiza wanachuo wote
kuendelea kutembelea ukurasa rasmi wa Instagram wa Seneti Mkoa wa Shinyanga ili
kupata taarifa mbalimbali, matangazo na shughuli zinazoendelea kufanywa na
Seneti hiyo.
Ziara ya viongozi wa Seneti Mkoa wa Shinyanga inaendelea katika vyuo mbalimbali mkoani humo ikiwa ni sehemu ya mpango wa kutembelea vyuo 17 kwa lengo la kuimarisha uongozi wa wanafunzi, kutoa elimu na kusikiliza changamoto zinazowakabili wanachuo.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Jackson Aloyce Mwizarubi akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Chuo cha Serikali za Mitaa, mjini Shinyanga.
Katibu wa Seneti Mkoa wa Shinyanga Lukomanga Jinyage
Jiboli akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Chuo cha
Serikali za Mitaa, mjini Shinyanga.

Katibu Hamasa wa Seneti, Sharon Callist Mathias naye akisaini
kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Chuo cha Serikali za Mitaa, mjini Shinyanga.
Viongozi wa Seneti Mkoa wa Shinyanga wakiwa katika mazungumzo mafupi na walimu wa Chuo cha Serikali za Mitaa kuhusu maendeleo ya wanachuo na ushirikiano wa kielimu.
Viongozi wa Seneti Mkoa wa Shinyanga wakiwa katika mazungumzo mafupi na walimu wa Chuo cha Serikali za Mitaa kuhusu maendeleo ya wanachuo na ushirikiano wa kielimu.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga akizungumza kwenye kikao hicho na walimu wa Chuo cha Serikali za Mitaa ikiwa ni sehemu ya ziara yao chuoni hapo.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga akizungumza kwenye kikao hicho na walimu wa Chuo cha Serikali za Mitaa ikiwa ni sehemu ya ziara yao chuoni hapo.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga akitoa shukrani kwa uongozi wa Chuo cha Serikali za Mitaa kwa ushirikiano waliouonyesha wakati wa ziara hiyo.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Jackson Aloyce Mwizarubi akizungumza na wanachuo katika ukumbi wa Chuo cha Serikali za Mitaa kuhusu uongozi, uzalendo na fursa za maendeleo kwa vijana.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga akitoa wito kwa wanachuo kuwa wabunifu, wenye nidhamu na wazalendo kwa taifa lao.
Katibu wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Lukomanga Jinyage Jiboli akitoa elimu kwa wanachuo kuhusu umuhimu wa kulinda amani na kudumisha mshikamano.
Katibu wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Lukomanga Jinyage Jiboli akitoa elimu kwa wanachuo kuhusu umuhimu wa kulinda amani na kudumisha mshikamano.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Jackson Aloyce Mwizarubi akiendelea kuzungumza na wanachuo kuhusu uongozi, uzalendo na fursa za maendeleo kwa vijana.
Wanachuo wa Chuo cha Serikali za Mitaa wakifuatilia kwa makini elimu inayotolewa na viongozi wa Seneti Mkoa wa Shinyanga.
Wanachuo wa Chuo cha Serikali za Mitaa wakifuatilia kwa makini elimu inayotolewa na viongozi wa Seneti Mkoa wa Shinyanga.
Wanachuo wa Chuo cha Serikali za Mitaa wakifuatilia kwa makini elimu inayotolewa na viongozi wa Seneti Mkoa wa Shinyanga.
Mwanafunzi wa Chuo cha Serikali za Mitaa akiuliza swali kuhusu fursa za ajira na namna vijana wanavyoweza kujiajiri baada ya masomo.
Mwanachuo wa Chuo cha Serikali za Mitaa akitoa maoni yake mbele ya viongozi wa Seneti Mkoa wa Shinyanga wakati wa mjadala chuoni hapo.
Mwanafunzi wa Chuo cha Serikali za Mitaa akiomba ufafanuzi kuhusu fursa mbalimbali zinazotolewa kwa vijana kupitia Seneti.
Mwanafunzi wa chuo hicho akiuliza swali kuhusu nafasi ya Seneti katika kutatua changamoto za wanachuo.
Mwanachuo akizungumza ukumbini wakati wa kipindi cha maswali na majibu kati ya wanafunzi na viongozi wa Seneti Mkoa wa Shinyanga.
Jackson Aloyce Mwizarubi akikabidhi kaunta book kwa Katibu wa Seneti tawi la Chuo cha Serikali za Mitaa ikiwa ni sehemu ya kuimarisha uongozi wa wanafunzi.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga akikabidhi faili kwa Mwenyekiti wa Seneti tawi la chuo hicho kwa ajili ya kurahisisha utendaji kazi wa viongozi wa wanafunzi.
Viongozi wa Seneti Mkoa wa Shinyanga wakiwa katika picha ya pamoja na wanachuo pamoja na viongozi wa Chuo cha Serikali za Mitaa mara baada ya kumalizika kwa ziara yao chuoni hapo.
Viongozi wa Seneti Mkoa wa Shinyanga wakiwa katika picha ya pamoja na wanachuo pamoja na viongozi wa Chuo cha Serikali za Mitaa mara baada ya kumalizika kwa ziara yao chuoni hapo.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Jackson Aloyce Mwizarubi akizungumza na wanachuo waliokuwa wakijisomea nje ya ukumbi, akiwahamasisha kuchangamkia fursa mbalimbali za maendeleo na ajira.
Jackson Aloyce Mwizarubi akitoa elimu ya fursa kwa baadhi ya wanachuo waliokutana naye nje ya ukumbi wakati wa ziara ya Seneti chuoni hapo.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga akizungumza na wanachuo waliokuwa wakijisomea nje, akisisitiza umuhimu wa elimu, nidhamu na kujiajiri.
Wanachuo waliokuwa wakijisomea nje wakisikiliza maelezo ya Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga kuhusu fursa zinazowazunguka vijana.
Katibu wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Lukomanga Jinyage Jiboli akizungumza na wanachuo nje ya ukumbi kuhusu umuhimu wa amani, nidhamu na mshikamano kwa vijana wa vyuo.
Lukomanga Jinyage Jiboli akitoa elimu kwa wanachuo waliokuwa nje ya ukumbi kuhusu nafasi ya vijana katika kulinda amani na maendeleo ya taifa.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Jackson Aloyce
Mwizarubi, akitoa elimu kwa wanachuo wa SHYCOM kuhusu uongozi, uzalendo na
umuhimu wa vijana kutumia fursa za elimu kujiletea maendeleo.
Mwanachuo wa SHYCOM akiuliza swali kuhusu nafasi ya vijana katika uongozi na maendeleo ya jamii wakati wa kikao cha elimu kilichoandaliwa na Seneti Mkoa wa Shinyanga.
Katibu Hamasa wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Sharon
Callist Mathias, akitoa hamasa kwa wanachuo wa SHYCOM kuhusu kujiamini, kutumia
fursa za elimu na kushiriki katika maendeleo ya jamii.
Katibu wa Seneti tawi la SHYCOM akipokea faili kutoka kwa Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga wakati wa ziara ya viongozi wa Seneti chuoni hapo.
Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga, Jackson Aloyce
Mwizarubi, akikabidhi kaunta book kwa Mwenyekiti wa Seneti tawi la SHYCOM ikiwa
ni sehemu ya kuimarisha utendaji na uongozi wa wanafunzi chuoni hapo.
Katibu wa Seneti tawi la chuo cha ST. Joseph akipokea faili kutoka kwa Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Shinyanga wakati wa ziara ya viongozi wa Seneti chuoni hapo.
Picha ya pamoja ya viongozi wa Seneti Mkoa wa
Shinyanga pamoja na wanachuo wa SHYCOM mara baada ya kikao cha elimu na hamasa
kilicholenga kuimarisha uongozi, uzalendo na maendeleo ya vijana.SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254






















Post a Comment