Na Mapuli Kitina Misalaba
Timu ya Bulige FC kutoka Wilaya ya Kahama imefanikiwa
kutinga hatua ya robo fainali ya mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 baada ya
kuibuka na ushindi wa penati 4-1 dhidi ya Manheigana FC katika mchezo mkali
uliochezwa leo Juni 11, 2026 kwenye Uwanja wa Mwabenda, Kata ya Solwa.
Mchezo huo ulimalizika kwa sare ya bila kufungana
ndani ya dakika 90 za kawaida, huku timu zote zikishindwa kutumia nafasi
walizozipata kutikisa nyavu.
Kutokana na sare hiyo, mshindi alitafutwa kwa mikwaju
ya penati ambapo Bulige FC ilionesha utulivu mkubwa na kufanikiwa kufunga penati
nne dhidi ya moja ya Manheigana FC, matokeo yaliyoifanya kutinga hatua
inayofuata ya mashindano hayo.
Akizungumza baada ya mchezo huo, kocha wa Bulige FC
ameushukuru uongozi wa mashindano pamoja na mashabiki wao kwa ushirikiano
waliouonesha, huku akiahidi kuwa timu hiyo itaendelea kupambana kwa bidii
katika hatua zinazofuata za mashindano.
Kwa upande wake, kocha wa Manheigana FC amepongeza
maandalizi ya mashindano hayo na kuushukuru uongozi wa NIACHEKONA CUP kwa
kuwapa nafasi ya kushiriki, akieleza kuwa licha ya kuondolewa wamejifunza mambo
mengi na watarejea wakiwa imara zaidi katika mashindano yajayo.
Katibu wa Kamati ya Mashindano ya NIACHEKONA CUP,
Sambayi Jilya, ametangaza kuwa mchezo wa kesho utawakutanisha Sangu FC na Kashishi
FC katika pambano linalotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa huku kila timu
ikisaka nafasi ya kusonga mbele.
Sambayi Jilya amewahimiza wananchi na wadau wa michezo
kuendelea kujitokeza kwa wingi katika Uwanja wa Mwabenda ili kushuhudia vipaji
mbalimbali vya vijana vinavyoendelea kuoneshwa kupitia mashindano hayo.
Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yameandaliwa na Bwana
Paul Daud Augustino maarufu MC NIACHEKONA kwa ufadhili wa Shirika la Lushu
Foundation, yakiwa na lengo la kuibua vipaji vya vijana, kukuza michezo,
kuimarisha mshikamano wa jamii na kudumisha amani.
Kwa mawasiliano ya shughuli mbalimbali za michezo, matangazo na ushereheshaji wa matukio, wasiliana na MC NIACHEKONA kupitia namba 0757 267 738.
Kikosi cha Manheigana FC.
Mchezo wa Bulige FC na Manheigana FC ukiendelea katika Uwanja wa Mwabenda kabla ya hatima yake kuamuliwa kwa mikwaju ya penati.
Mchezo wa Bulige FC na Manheigana FC ukiendelea katika Uwanja wa Mwabenda kabla ya hatima yake kuamuliwa kwa mikwaju ya penati.
Viongozi wa mashindano na wadau wa michezo wakishuhudia ushindani mkubwa kati ya Bulige FC na Manheigana FC mbele ya mamia ya mashabiki waliojitokeza uwanjani leo Juni 11, 2026.
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254
















































Post a Comment