" KIMANDAGULI FC NA ISENENGEJA FC ZAONDOLEWA NIACHEKONA CUP 2026 KWA KUKIUKA KANUNI ZA MASHINDANO

KIMANDAGULI FC NA ISENENGEJA FC ZAONDOLEWA NIACHEKONA CUP 2026 KWA KUKIUKA KANUNI ZA MASHINDANO

Na Mapuli Kitina Misalaba

Kamati ya Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 imeziondoa timu mbili kwenye mashindano hayo kutokana na ukiukwaji wa kanuni na taratibu zilizowekwa kabla ya kuanza kwa ligi hiyo.

Akisoma taarifa kwa niaba ya Kamati ya Mashindano, Makamu Mwenyekiti wa NIACHEKONA CUP, Bwana Samwel Stephen, amesema timu ya Kimandaguli FC imeondolewa kwenye mashindano hayo kwa sababu za kinidhamu baada ya baadhi ya mashabiki wake pamoja na benchi la ufundi kuhusika katika vitendo vya fujo wakati wa mchezo.

Amesema pamoja na Kimandaguli FC kufanikiwa kufuzu na kuingia hatua ya timu 12 bora, kamati imelazimika kuchukua hatua hiyo kwa lengo la kulinda nidhamu, amani na heshima ya mashindano hayo.

Bwana Samwel Stephen amesema pia kuwa timu ya Isenengeja FC kutoka Wilaya ya Misungwi imeondolewa kwenye mashindano hayo baada ya kukiuka mara mbili kanuni za mashindano zinazohusu muda wa kufika uwanjani.

Ameeleza kuwa mara ya kwanza kamati ilitoa onyo kwa timu hiyo baada ya kuchelewa kufika kwenye mchezo wake, lakini ilirudia kosa hilo kwa mara nyingine ambapo ilifika uwanjani majira ya saa kumi na moja jioni, jambo ambalo limeonekana kuhatarisha ratiba ya mashindano.

Makamu Mwenyekiti huyo amezitaka timu zote zilizosalia kwenye mashindano hayo kuendelea kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa ili kuhakikisha mashindano yanaendelea kwa amani, nidhamu na ushindani wa haki.

Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yameandaliwa na Bwana Paul Daud Augustino maarufu MC NIACHEKONA kwa lengo la kuibua vipaji vya vijana, kukuza michezo na kuimarisha mshikamano katika jamii.

Kwa mawasiliano ya huduma za ushereheshaji wa shughuli mbalimbali, matangazo na matukio ya kijamii, MC NIACHEKONA anapatikana kupitia namba 0757 267 738.

Kikosi cha ISENENGEJA FC.

 SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment

Previous Post Next Post