" MASHABIKI WA HOME BOYS WATABIRI USHINDI WA MAGOLI 10 DHIDI YA UFUKUNYUNGU FC

MASHABIKI WA HOME BOYS WATABIRI USHINDI WA MAGOLI 10 DHIDI YA UFUKUNYUNGU FC

Baadhi ya mashabiki wa timu ya Home Boys FC kutoka Kata ya Solwa wameonesha kujiamini kuelekea mchezo wa leo dhidi ya Ufukunyungu FC kutoka Ngokolo, Manispaa ya Shinyanga, kwa kutabiri ushindi mnono wa timu yao.

Wakizungumza na Misalaba Media, mashabiki hao wamesema wana imani kubwa na kikosi cha Home Boys FC kutokana na kiwango kizuri walichoonesha katika michezo iliyopita, huku baadhi yao wakitabiri timu hiyo kuibuka na ushindi wa hadi magoli 10 dhidi ya wapinzani wao.

Wamesema wanaamini uwepo wa kocha mpya pamoja na morali kubwa ya wachezaji utasaidia timu hiyo kufanya vizuri na kutinga hatua inayofuata ya mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026.

Hata hivyo, mashabiki hao wamewataka wachezaji wa Home Boys FC kutobweteka na badala yake kuingia uwanjani kwa nidhamu, kujituma na kupambana ili kutimiza matarajio ya mashabiki wao.

Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa katika Uwanja wa Mwabenda huku ukitarajiwa kuvutia mashabiki wengi kutoka Solwa, Ngokolo na maeneo mengine ya Mkoa wa Shinyanga.

 SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment

Previous Post Next Post