" MAWEMIRU FC YAONESHA UBABE BAADA YA KUFUZU KWA PENATI, BAJAJI FC NA NYANDOLWA FC KUKIPIGA KESHO

MAWEMIRU FC YAONESHA UBABE BAADA YA KUFUZU KWA PENATI, BAJAJI FC NA NYANDOLWA FC KUKIPIGA KESHO


Na Mapuli Kitina Misalaba

Timu ya MAWEMIRU FC imefanikiwa kutinga hatua inayofuata ya mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 baada ya kuiondoa MAHEMBE FC kwa mikwaju ya penati katika mchezo wa marudiano uliochezwa katika uwanja wa Mwabenda, kata ya Solwa, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.

Mchezo huo uliokuwa na ushindani mkubwa ulimalizika kwa ushindi wa penati 4-2 kwa MAWEMIRU FC baada ya timu hizo kushindwa kupata mshindi ndani ya dakika 90 za kawaida.

Ikumbukwe kuwa katika mchezo wa kwanza, MAWEMIRU FC ilifungwa bao 1-0 na MAHEMBE FC, hivyo kuingia uwanjani leo Mei 1, 2026 ikiwa na jukumu la kusawazisha matokeo hayo ili kuendelea kusalia kwenye mashindano.

Katika dakika 90 za mchezo wa leo, MAWEMIRU FC ilifanikiwa kupata bao moja muhimu lililofanya matokeo ya jumla ya michezo yote miwili kuwa sare, hali iliyolazimu mshindi kupatikana kwa mikwaju ya penati kwa mujibu wa kanuni za mashindano hayo.

Kwa ushindi huo, MAWEMIRU FC sasa itakutana na NYUNDO FC katika hatua inayofuata ya mashindano hayo, baada ya NYUNDO FC kufuzu jana kwa kuiondoa NZOZA FC kwa mikwaju ya penati.

Akizungumza baada ya mchezo huo, Makamu Mwenyekiti wa NIACHEKONA CUP, Bwana Samwel Stephen ametangaza ratiba ya mchezo wa kesho ambapo BAJAJI FC itamenyana na NYANDOLWA FC katika pambano linalotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.

Ameendelea kuwahimiza wananchi, wadau wa michezo na mashabiki wa soka kujitokeza kwa wingi katika uwanja wa Mwabenda ili kuendelea kushuhudia vipaji vya vijana pamoja na burudani ya michezo inayotolewa kupitia mashindano hayo.

Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yameandaliwa na Paul Daud Augustino (MC NIACHEKONA) kwa ufadhili wa shirika la Lushu Foundation yakiwa na lengo la kuibua vipaji vya vijana, kukuza michezo, kuimarisha amani na kuchochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Kwa huduma za ushereheshaji wa matukio mbalimbali, matangazo na burudani, MC NIACHEKONA anapatikana kupitia namba 0757 267 738.

Kikosi cha Mawemiru FC

 SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment

Previous Post Next Post