Na Mapuli Kitina Misalaba
Mtendaji wa Kata ya Solwa, Jackson Maganga, amewahimiza
wananchi na mashabiki wanaofika uwanjani kuendelea kudumisha amani, utulivu na
kuheshimu sheria na taratibu zilizowekwa ili mashindano hayo yaendelee
kufanyika katika mazingira salama.
Maganga amempongeza mwandaaji wa mashindano ya
NIACHEKONA CUP 2026, Bwana Paul Daud Augustino maarufu MC NIACHEKONA, kwa
kuandaa mashindano hayo ambayo amesema yamekuja wakati muafaka kwa wananchi wa
kata hiyo.
Amesema kwa sasa wananchi wengi wa Solwa wanaendelea
na shughuli za mavuno, hivyo amewahimiza kutumia muda wa asubuhi na mchana
kufanya kazi za kilimo huku wakitumia nyakati za jioni kufuatilia burudani ya
soka kupitia mashindano ya NIACHEKONA CUP yanayofanyika katika uwanja wa
Mwabenda.
Amesema mashindano hayo yamekuwa sehemu ya burudani,
mshikamano na kuwakutanisha wananchi kutoka maeneo mbalimbali, huku yakitoa
fursa kwa vijana kuonesha vipaji vyao.
Maganga amewahakikishia wananchi kuwa serikali
itaendelea kushirikiana na waandaaji wa mashindano hayo, akieleza kuwa ina
imani na jitihada zinazofanywa na MC NIACHEKONA katika kukuza michezo na
kuhamasisha maendeleo ya vijana pamoja na jamii kwa ujumla.
Amewahimiza wananchi wa Solwa na maeneo jirani
kuendelea kujitokeza kwa wingi katika uwanja wa Mwabenda kushuhudia michezo
mbalimbali ya NIACHEKONA CUP 2026.
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254
Post a Comment