" NYUNDO FC YAAGA MASHINDANO YA NIACHEKONA CUP 2026, MAWEMIRU FC YAENDELEA KUWASHA MOTO

NYUNDO FC YAAGA MASHINDANO YA NIACHEKONA CUP 2026, MAWEMIRU FC YAENDELEA KUWASHA MOTO

Na Mapuli Kitina Misalaba

Timu ya MAWEMIRU FC imefanikiwa kutinga hatua inayofuata katika mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 baada ya kuiondoa NYUNDO FC kwa ushindi wa penati 4-3 kwenye mchezo ambao umechezwa katika uwanja wa Mwabenda, kata ya Solwa, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.

Mchezo huo uliokuwa na ushindani mkubwa ulimalizika kwa sare ya bao 1-1 ndani ya dakika 90 za kawaida, hali iliyolazimu mshindi kupatikana kwa mikwaju ya penati kwa mujibu wa kanuni za mashindano hayo.

Katika kipindi cha kwanza, MAWEMIRU FC ilifanikiwa kupata bao moja lililowapa matumaini ya kuendelea kutafuta ushindi. Hata hivyo, NYUNDO FC walirejea kwa nguvu kipindi cha pili na kufanikiwa kusawazisha bao hilo, na kufanya mchezo huo kumalizika kwa sare ya bao 1-1.

Baada ya sare hiyo, timu hizo zilielekea katika hatua ya mikwaju ya penati ambapo MAWEMIRU FC ilionesha umakini mkubwa na kufanikiwa kushinda kwa penalti 4-3, ushindi uliowapa nafasi ya kusonga mbele huku ukiihitimisha safari ya NYUNDO FC katika mashindano hayo ya mwaka 2026.

Viongozi na mashabiki wa NYUNDO FC wameishukuru Kamati ya Mashindano pamoja na mwandaaji wa ligi hiyo kwa kuwapa nafasi ya kushiriki mashindano hayo huku wakiahidi kurejea kwa nguvu zaidi katika mashindano yajayo.

Akizungumza katibu wa Mashindano ya NIACHEKONA CUP, Sambayi Jilya ametangaza ratiba ya mchezo unaotarajiwa kuchezwa kesho ambapo Duara FC itamenyana na Songambele Mhangu FC katika pambano linalotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana na ubora wa timu hizo katika mashindano yanayoendelea.

Amewahimiza wananchi, wadau wa michezo na mashabiki wa soka kujitokeza kwa wingi katika uwanja wa Mwabenda ili kushuhudia burudani ya soka pamoja na kuendelea kuunga mkono juhudi za kuibua vipaji vya vijana kupitia mashindano hayo.

Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yameandaliwa na Bwana Paul Daud Augustino maarufu MC NIACHEKONA kwa ufadhili wa shirika la Lushu Foundation, yakiwa na lengo la kuibua vipaji vya vijana, kuimarisha amani, kukuza michezo na kuchochea maendeleo ya kijamii.

Kwa mawasiliano ya huduma za ushereheshaji wa shughuli mbalimbali, matangazo na matukio ya kijamii, MC NIACHEKONA anapatikana kupitia namba 0757 267 738.

NIACHEKONA CUP MWABENDA – WEKA TU WEKE.




SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254




 

Post a Comment

Previous Post Next Post