" PARAGUAY YAITUPA NJE UJERUMANI KOMBE LA DUNIA 2026

PARAGUAY YAITUPA NJE UJERUMANI KOMBE LA DUNIA 2026

 


Timu ya taifa ya Paraguay imefanikiwa kuitoa Ujerumani katika mashindano ya Kombe la Dunia baada ya kushinda kwa mikwaju ya penalti 4-3, kufuatia sare ya 1-1 iliyodumu kwa dakika 120 katika mchezo wa hatua ya 32 bora.

Kwa matokeo hayo, Paraguay imetinga hatua ya 16 bora kwa mara ya tano katika historia yake. Ushindi huo pia umeonekana kuwa kisasi kitamu baada ya kusubiri kwa miaka 24.

Ikumbukwe kuwa mwaka 2002, nchini Korea Kusini na Japan, Ujerumani iliiondoa Paraguay katika hatua hiyo kwa ushindi wa bao 1-0, lililofungwa mwishoni mwa mchezo na Oliver Neuville. Safari hii, hata hivyo, Paraguay imeandika historia mpya kwa kuiondoa Ujerumani na kufuzu hatua inayofuata.

SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment

Previous Post Next Post