Baada ya uzinduzi wa kampeni ya “Bonge la Wakala”
uliofanyika katika Tawi la Benki ya CRDB Shinyanga, mawakala wa benki hiyo
wameanza kuwafikia wananchi katika maeneo mbalimbali ya Manispaa ya Shinyanga
kwa lengo la kuwapatia elimu ya huduma za kifedha na namna ya kunufaika na
fursa zilizopo kupitia kampeni hiyo.
Mawakala hao wametembelea maeneo mbalimbali ya
biashara na makazi ikiwemo Soko la Nguzonane, Soko la Kambarage, Lubaga, Soko
Kuu la Shinyanga, Stendi ya Mkoa (Manyoni), Kitangili maeneo ya mashine za
kukoboa mpunga, Stendi ya Zamani pamoja na mitaa mbalimbali ya Ngokolo.
Katika ziara hiyo, wananchi walipata nafasi ya
kufahamishwa kuhusu huduma zinazotolewa kupitia CRDB Wakala, faida za kufanya
miamala ya kibenki karibu na maeneo yao pamoja na fursa za kushiriki kampeni ya
“Bonge la Wakala” inayotoa zawadi mbalimbali kwa mawakala na wateja wa benki
hiyo.
Akizungumza wakati wa shughuli hizo, Meneja wa Benki
ya CRDB Kanda ya Magharibi, Jumanne Wagana, amesema kampeni hiyo inalenga
kuongeza matumizi ya huduma za mawakala, kuimarisha ujumuishaji wa kifedha na
kuwahamasisha wananchi kutumia huduma za kibenki kwa urahisi zaidi.
Amesema mawakala wameendelea kuwa sehemu muhimu ya
utoaji wa huduma za kifedha kwa kuwafikishia wananchi huduma karibu na maeneo
yao, hali inayosaidia kupunguza msongamano katika matawi ya benki na kuongeza
upatikanaji wa huduma kwa wakati.
Mbali na utoaji wa elimu, shughuli hizo zilipambwa na
burudani kutoka kikundi cha Kambi ya Nyani, ambacho kilitoa burudani katika
kila eneo lililotembelewa na kuvutia wananchi kujitokeza kwa wingi kusikiliza
elimu iliyokuwa ikitolewa na mawakala wa CRDB.
Wananchi waliopata elimu hiyo wameeleza kufurahishwa
na hatua ya benki hiyo kusogeza huduma na elimu ya kifedha karibu nao, huku
wakiahidi kutumia kikamilifu fursa zinazotolewa kupitia kampeni ya “Bonge la
Wakala”.
Kampeni hiyo inaendelea katika maeneo mbalimbali ikiwa na lengo la kuwafikia wananchi wengi zaidi, kuongeza matumizi ya huduma za kidigitali na kuhamasisha ukuaji wa biashara za mawakala wa CRDB nchini.
Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi, Jumanne Wagana, akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Bonge la Wakala uliofanyika leo Juni 25, 2026 mjini Shinyanga.


Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi, Jumanne Wagana, akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Bonge la Wakala uliofanyika leo Juni 25, 2026 mjini Shinyanga.

Meneja wa Benki ya CRDB Tawi la Shinyanga, Luther Mneney, akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Bonge la Wakala uliofanyika leo Juni 25, 2026 mjini Shinyanga.
Meneja wa Benki ya CRDB Tawi la Shinyanga, Luther Mneney, akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Bonge la Wakala uliofanyika leo Juni 25, 2026 mjini Shinyanga.
Meneja wa Benki ya CRDB Tawi la Shinyanga, Luther Mneney, akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Bonge la Wakala uliofanyika leo Juni 25, 2026 mjini Shinyanga.
Meneja wa Biashara wa Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi, Anselm Mwenda, akizungumza na mawakala wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Bonge la Wakala
Wakala wa CRDB akitoa elimu kwa wafanyabiashara wa Soko la Nguzonane kuhusu huduma za CRDB Wakala na fursa zinazopatikana kupitia kampeni ya Bonge la Wakala.
Wakala wa CRDB akitoa elimu kwa wafanyabiashara wa Soko la Nguzonane kuhusu huduma za CRDB Wakala na fursa zinazopatikana kupitia kampeni ya Bonge la Wakala.
Wakala wa CRDB akimhudumia mteja katika eneo la Soko la Kambarage huku akiendelea kuhamasisha matumizi ya huduma za kifedha kupitia CRDB Wakala.
Wakala wa CRDB akimhudumia mteja katika eneo la Soko la Kambarage huku akiendelea kuhamasisha matumizi ya huduma za kifedha kupitia CRDB Wakala.
Wakala wa CRDB akimhudumia mteja katika eneo la Soko la Kambarage huku akiendelea kuhamasisha matumizi ya huduma za kifedha kupitia CRDB Wakala.
Wakala wa CRDB akizungumza na wafanyabiashara wa Soko Kuu la Shinyanga kuhusu faida za kufanya miamala kupitia CRDB Wakala.
Wakala wa CRDB akizungumza na wafanyabiashara wa Soko Kuu la Shinyanga kuhusu faida za kufanya miamala kupitia CRDB Wakala.
Wakala wa CRDB akizungumza na wafanyabiashara wa Soko Kuu la Shinyanga kuhusu faida za kufanya miamala kupitia CRDB Wakala.
Makala wa CRDB akizungumza na wafanyabiashara wa Soko Kuu la Shinyanga kuhusu faida za kufanya miamala kupitia CRDB Wakala.
Wakala wa CRDB akizungumza na wafanyabiashara wa Soko Kuu la Shinyanga kuhusu faida za kufanya miamala kupitia CRDB Wakala.
Wakala wa CRDB akitoa maelezo kwa mwananchi katika Stendi ya Mkoa wa Shinyanga (Manyoni) kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa kupitia CRDB Wakala.
Wakala wa CRDB akitoa maelezo kwa mwananchi katika Stendi ya Mkoa wa Shinyanga (Manyoni) kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa kupitia CRDB Wakala.
Wakala wa CRDB akitoa maelezo kwa mwananchi katika Stendi ya Mkoa wa Shinyanga (Manyoni) kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa kupitia CRDB Wakala.
Wakala wa CRDB akitoa maelezo kwa mwananchi katika Stendi ya Mkoa wa Shinyanga (Manyoni) kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa kupitia CRDB Wakala.
Wakala wa CRDB akitoa maelezo kwa wananchi katika Stendi ya Mkoa wa Shinyanga (Manyoni) kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa kupitia CRDB Wakala.
Wakala wa CRDB akitoa maelezo kwa mwananchi katika Stendi ya Mkoa wa Shinyanga (Manyoni) kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa kupitia CRDB Wakala.
Wakala wa CRDB akitoa elimu kwa wajasiriamali na wakazi wa Kitangili eneo la mashine za kukoboa mpunga kuhusu fursa za huduma za kifedha.
Wakala wa CRDB akitoa elimu kwa wajasiriamali na wakazi wa Kitangili eneo la mashine za kukoboa mpunga kuhusu fursa za huduma za kifedha.
Wakala wa CRDB akitoa elimu kwa wajasiriamali na wakazi wa Kitangili eneo la mashine za kukoboa mpunga kuhusu fursa za huduma za kifedha.
Wakala wa CRDB akitoa elimu kwa mjasiriamali mkazi wa Kitangili eneo la mashine za kukoboa mpunga kuhusu fursa za huduma za kifedha.
Wakala wa CRDB wakiwahudumia wananchi katika Stendi ya Zamani wakati wa zoezi la uhamasishaji wa kampeni ya Bonge la Wakala.
Wakala wa CRDB akiwahudumia wananchi katika Stendi ya Zamani wakati wa zoezi la uhamasishaji wa kampeni ya Bonge la Wakala.
Mwananchi wa Ngokolo akisikiliza elimu ya huduma za CRDB Wakala iliyotolewa na mawakala wa benki hiyo katika mwendelezo wa kampeni ya Bonge la Wakala.SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254
























































Post a Comment