
Na Mapuli Kitina Misalaba
Timu ya Ufukunyungu FC kutoka Manispaa ya Shinyanga imefanikiwa kutinga hatua ya fainali ya mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 baada ya kuibuka na ushindi wa mikwaju ya penati dhidi ya Duara FC katika mchezo wa nusu fainali uliochezwa katika Uwanja wa Mwabenda, Kata ya Solwa, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.
Ndani ya dakika 90 za mchezo huo, timu hizo zilitoka
sare ya goli 1-1. Ufukunyungu FC ndiyo ilikuwa ya kwanza kupata bao katika
kipindi cha kwanza kabla ya Duara FC kusawazisha kipindi cha pili na kufanya
mchezo huo kumalizika kwa sare.
Matokeo hayo yalizifanya timu hizo kwenda kwenye
mikwaju ya penati ambapo Ufukunyungu FC ilionyesha utulivu mkubwa na kufanikiwa
kushinda kwa penalti 5-4, ushindi ulioihakikishia nafasi ya kucheza fainali ya
mashindano hayo.
Kwa ushindi huo, Ufukunyungu FC imekuwa timu ya kwanza
kufuzu fainali na sasa inamsubiri mshindi wa mchezo wa kesho wa nusu fainali
kati ya Bulige FC na Kashishi FC ili kujua mpinzani wake wa mwisho katika mbio
za ubingwa.
Kwa upande wa Duara FC, bado ina nafasi ya kumaliza
katika nafasi ya tatu, ambapo itacheza na timu itakayofungwa katika mchezo wa
kesho wa nusu fainali.
Akizungumza baada ya mchezo huo, Katibu wa Kamati ya
Mashindano, Sambayi Jilya, ametangaza kuwa mchezo wa pili wa nusu fainali
utachezwa kesho ukizikutanisha Bulige FC na Kashishi FC katika pambano la
kusaka tiketi ya pili ya kucheza fainali.
Aidha, ratiba ya fainali tayari imetangazwa ambapo
siku ya Jumanne, Juni 23, 2026, kutakuwa na mchezo wa kusaka mshindi wa tatu
kuanzia saa nane mchana, huku mchezo wa fainali ukitarajiwa kuanza saa kumi
jioni.
Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yameandaliwa na Paul
Daud Augustino maarufu MC NIACHEKONA kwa ufadhili wa Shirika la Lushu
Foundation, yakilenga kuibua vipaji vya vijana, kukuza michezo na kuimarisha
mshikamano wa jamii.
Kwa huduma za MC, matangazo na ushereheshaji wa matukio mbalimbali, wasiliana na MC NIACHEKONA kupitia namba 0757 267 738.
Kikosi cha Duara FC na sabu.
Wachezaji wa Ufukunyungu FC na Duara FC wakionyesha ushindani mkubwa katika pambano la nusu fainali leo Juni 18, 2026.
Viongozi wa mashindano na wadau wa michezo wakifuatilia kwa karibu mchezo wa nusu fainali kati ya Ufukunyungu FC na Duara FC leo Juni 18, 2026.
Viongozi wa mashindano na wadau wa michezo wakifuatilia kwa karibu mchezo wa nusu fainali kati ya Ufukunyungu FC na Duara FC.
Mashabiki na wananchi waliojitokeza kwa wingi kushuhudia mchezo wa nusu fainali ya NIACHEKONA CUP 2026.

Mashabiki na wananchi waliojitokeza kwa wingi kushuhudia mchezo wa nusu fainali ya NIACHEKONA CUP 2026.SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254




























































Post a Comment