Na Mapuli
Kitina Misalaba
Diwani wa
Kata ya Solwa, Mhe. Dotto Samson maarufu kwa jina la Ipililo, leo Juni 15, 2026
amefanya mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Solwa chenye vitongoji vitano,
ambapo amewahimiza wananchi kuendelea kudumisha amani, umoja na utulivu huku
akiahidi kuendelea kupigania maendeleo ya kijiji hicho na Kata ya Solwa kwa
ujumla.
Akizungumza
katika mkutano huo uliofanyika kijijini hapo, Mhe. Ipililo amesema kuwa
maendeleo hayawezi kupatikana bila kuwepo kwa amani na ushirikiano kati ya
wananchi na viongozi, hivyo amewataka wakazi wa Solwa kuendelea kuwa walinzi wa
amani na mshikamano uliopo katika eneo lao.
Amesema
mkutano huo ni sehemu ya mwendelezo wa ziara zake za kutembelea vijiji
mbalimbali vya Kata ya Solwa kwa lengo la kuwashukuru wananchi kwa imani kubwa
waliyoionesha kwake wakati wa uchaguzi mdogo uliofanyika kufuatia kifo cha
aliyekuwa Diwani wa kata hiyo.
Katika
mkutano huo, Diwani huyo pia amelipongeza Jeshi la Jadi Sungusungu kwa mchango
wake katika kuimarisha ulinzi na usalama wa wananchi, huku akiwataka kuendelea
kushirikiana na Serikali pamoja na vyombo vya dola katika kulinda amani ya
maeneo yao.
Aidha,
amewasisitiza viongozi wa jeshi hilo wanaofahamika kama Watemi kuwa waadilifu,
wa mfano mzuri kwa jamii na kuendelea kuyaongoza majesho yao kwa kuzingatia
sheria, maadili na maslahi ya wananchi.
Mkutano huo
wa hadhara pia uliwapa wananchi fursa ya kueleza kero, changamoto na malalamiko
mbalimbali yanayowakabili katika maisha yao ya kila siku. Baadhi ya wananchi
waliwasilisha maombi ya kuboreshwa kwa huduma za usafi wa mazingira, ikiwemo
kutengenezwa kwa dampo maalum la kutupia taka ili kuimarisha afya na usafi wa
mazingira katika kijiji hicho.
Kwa upande
wake, Mwenyekiti wa Kijiji cha Solwa, Bwana John Bernard Kaselya, akizungumza
kwa niaba ya wananchi, ameeleza kuwa pamoja na jitihada zinazofanywa na
Serikali, bado kijiji hicho kinakabiliwa na changamoto mbalimbali zinazohitaji
ufumbuzi wa haraka.
Ametaja
baadhi ya changamoto hizo kuwa ni ubovu wa miundombinu ya barabara katika
maeneo mbalimbali ya kijiji, bei ya maji, upatikanaji wa huduma ya maji safi na
salama pamoja na changamoto ya umeme katika baadhi ya vitongoji ambavyo bado
havijafikiwa kikamilifu na huduma hiyo.
Akijibu hoja
na maswali yaliyoulizwa na wananchi, Mhe. Ipililo amesema ataendelea
kuzifikisha changamoto zote katika mamlaka zinazohusika ili ziweze kupatiwa
ufumbuzi kwa wakati.
Amesema
tayari Serikali imepeleka na kupokea kiasi cha takribani shilingi milioni 10
kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya stendi ya Solwa, ikiwemo ukarabati wa
vyoo pamoja na kuziba mashimo na mabonde yaliyokuwa yakisababisha usumbufu kwa
watumiaji wa eneo hilo.
Vilevile,
amesema kupitia Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Wilaya ya
Shinyanga, tayari mchakato wa kuboresha barabara inayotoka Solwa Senta kupitia
Zahanati ya Ipililo umeidhinishwa, jambo ambalo litasaidia kupunguza changamoto
ya usafiri na usafirishaji iliyokuwa ikiwakabili wananchi kwa muda mrefu.
Diwani huyo
ameongeza kuwa ataandaa kamati maalum itakayoshirikiana na viongozi wa vijiji
na wananchi kufuatilia changamoto nyingine zilizobainishwa ili kuhakikisha
zinapatiwa ufumbuzi kwa haraka.
Ziara hiyo
ya Mhe. Ipililo imeambatana na wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Chama Cha
Mapinduzi (CCM) Kata ya Solwa. Mkutano huo pia umehudhuriwa na viongozi
mbalimbali pamoja na wataalamu kutoka ofisi ya kata, akiwemo Afisa Mifugo,
Afisa Maendeleo ya Jamii, Mganga Mfawidhi na Afisa Afya wa kata, ambao wamepata
nafasi ya kujibu maswali na kutoa ufafanuzi kuhusu huduma mbalimbali
zinazotolewa katika sekta zao.
Ushiriki wa wananchi kwa wingi pamoja na uwepo wa watu wenye mitazamo tofauti ya kisiasa katika mkutano huo umeelezwa kuwa ni ishara ya kuendelea kuimarika kwa mshikamano, uvumilivu wa kisiasa na ushirikiano katika Kijiji cha Solwa, hali ambayo ni muhimu katika kuharakisha maendeleo ya wananchi na taifa kwa ujumla.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Solwa, John Bernard Kaselya, akieleza changamoto zinazowakabili wananchi wa kijiji hicho mbele ya Diwani wa Kata ya Solwa na viongozi mbalimbali waliohudhuria mkutano wa hadhara.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Solwa, John Bernard Kaselya, akieleza changamoto zinazowakabili wananchi wa kijiji hicho mbele ya Diwani wa Kata ya Solwa na viongozi mbalimbali waliohudhuria mkutano wa hadhara.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Solwa, John Bernard Kaselya, akieleza changamoto zinazowakabili wananchi wa kijiji hicho mbele ya Diwani wa Kata ya Solwa na viongozi mbalimbali waliohudhuria mkutano wa hadhara.
Diwani wa Kata ya Solwa, Mhe. Dotto Samson maarufu Ipililo, akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Solwa wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika Juni 15, 2026 kwa lengo la kusikiliza kero za wananchi, kuwashukuru kwa imani yao na kuzungumzia maendeleo ya kata hiyo.
Diwani wa Kata ya Solwa, Mhe. Dotto Samson maarufu Ipililo, akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Solwa wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika Juni 15, 2026 kwa lengo la kusikiliza kero za wananchi, kuwashukuru kwa imani yao na kuzungumzia maendeleo ya kata hiyo.
Diwani wa Kata ya Solwa, Mhe. Dotto Samson maarufu Ipililo, akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Solwa wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika Juni 15, 2026 kwa lengo la kusikiliza kero za wananchi, kuwashukuru kwa imani yao na kuzungumzia maendeleo ya kata hiyo.
Mmoja wa wakazi wa Kijiji cha Solwa akiwasilisha kero na maoni yake mbele ya Diwani wa Kata ya Solwa, Mhe. Dotto Samson (Ipililo), wakati wa mkutano wa hadhara ambao umefanyika leo Juni 15, 2026.
Mkazi wa Kijiji cha Solwa akiuliza swali kuhusu changamoto za maendeleo katika eneo lake wakati wa mkutano wa hadhara
Mmoja wa wananchi wa Kijiji cha Solwa akitoa hoja kuhusu huduma za kijamii mbele ya viongozi wa kata na wataalamu mbalimbali waliohudhuria mkutano huo.
Mkazi wa Solwa akiwasilisha maoni yake kuhusu maendeleo ya kijiji wakati wa mkutano wa hadhara uliohusisha wananchi, viongozi na wataalamu wa sekta mbalimbali.
Mwanachama wa CHADEMA akitoa maoni na kuwasilisha hoja zake wakati wa mkutano wa hadhara hali iliyoonesha uwepo wa demokrasia, umoja na mshikamano miongoni mwa wananchi.
Mmoja wa wananchi wa Kijiji cha Solwa akitoa hoja yake wakati wa mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na Diwani wa Kata ya Solwa, viongozi wa CCM na wataalamu wa kata.
Baadhi ya
wananchi wa Kijiji cha Solwa wakifuatilia mkutano wa hadhara ambapo masuala ya
maendeleo, amani na changamoto mbalimbali za wananchi yamejadiliwa.

Baadhi ya
wananchi wa Kijiji cha Solwa wakifuatilia mkutano wa hadhara ambapo masuala ya
maendeleo, amani na changamoto mbalimbali za wananchi yamejadiliwa.

Baadhi ya
wananchi wa Kijiji cha Solwa wakifuatilia mkutano wa hadhara ambapo masuala ya
maendeleo, amani na changamoto mbalimbali za wananchi yamejadiliwa.

Baadhi ya
wananchi wa Kijiji cha Solwa wakifuatilia mkutano wa hadhara ambapo masuala ya
maendeleo, amani na changamoto mbalimbali za wananchi yamejadiliwa.

Baadhi ya
wananchi wa Kijiji cha Solwa wakifuatilia mkutano wa hadhara ambapo masuala ya
maendeleo, amani na changamoto mbalimbali za wananchi yamejadiliwa.
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254



















































Post a Comment