" WANANCHI NA WADAU WA SOKA WAALIKWA KUSHUHUDIA (FAINALI ) KILELE CHA NIACHEKONA CUP 2026

WANANCHI NA WADAU WA SOKA WAALIKWA KUSHUHUDIA (FAINALI ) KILELE CHA NIACHEKONA CUP 2026

Na Mapuli Kitina Misalaba

Mkurugenzi wa mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026, Paul Daud Augustino maarufu MC NIACHEKONA, amewaalika wananchi, wadau wa michezo na wapenda soka kutoka maeneo mbalimbali kujitokeza kwa wingi kushuhudia kilele cha mashindano hayo kitakachofanyika kesho Jumanne, Juni 23, 2026, katika Uwanja wa Mwabenda, Kata ya Solwa, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.

Akizungumza kuelekea mchezo wa fainali, MC NIACHEKONA amesema shughuli za siku hiyo zitaanza mapema kwa mchezo wa kusaka mshindi wa tatu utakaozikutanisha Bulige FC na Duara FC (Mwabenda) kuanzia saa nane kamili mchana.

Amesema baada ya mchezo huo kutakuwa na burudani mbalimbali zitakazotolewa na vikundi na wasanii tofauti, ikiwemo Kundi la Dancers Kambi ya Nyani, kikundi cha tarumbeta pamoja na wasanii wa nyimbo za asili, kwa lengo la kuwapa burudani wananchi watakaohudhuria siku hiyo.

MC NIACHEKONA amesema saa kumi kamili jioni atawasili mgeni rasmi wa mashindano hayo, Mhe. Masalu Nyese, Diwani wa Kata ya Mwakitolyo, ambaye amealikwa kutokana na mchango wake katika maendeleo ya michezo na vijana.

Ameeleza kuwa uwepo wa mgeni rasmi utatoa fursa ya kuzungumza na vijana na wadau wa michezo kuhusu namna ya kuendeleza vipaji, kuhamasisha ushirikiano pamoja na kufikisha ujumbe kwa serikali na wadau wengine ili kuendelea kuimarisha sekta ya michezo.

Kwa mujibu wa MC NIACHEKONA, shughuli za itifaki zitasimamiwa na MC Dizzo, ambaye atakuwa na jukumu la kumkaribisha mgeni rasmi pamoja na wageni wengine waalikwa kabla ya kuanza kwa mchezo wa fainali.

Mchezo wa fainali utawakutanisha Ufukunyungu FC kutoka Manispaa ya Shinyanga na Kashishi FC kutoka Kata ya Solwa, timu mbili zilizofanikiwa kuzishinda timu nyingine 20 na kufuzu hatua ya mwisho kati ya timu 22 zilizoshiriki mashindano hayo mwaka huu.

Ameongeza kuwa mshindi wa kwanza atazawadiwa Kombe pamoja na shilingi milioni 1.2, huku mshindi wa pili akipata shilingi laki 6 na mshindi wa tatu shilingi laki 3.

Pia kutakuwa na tuzo mbalimbali za binafsi na timu, ambapo mchezaji bora, golikipa bora na mfungaji bora kila mmoja atapata shilingi elfu 50,000. Aidha, timu yenye nidhamu bora nayo itatunukiwa zawadi maalum kwa kutambua umuhimu wa kuzingatia maadili na sheria za mashindano.

MC NIACHEKONA amesema mgeni rasmi ameziarika timu zote zilizoshiriki mashindano hayo ili kuhudhuria siku ya fainali kwa ajili ya kupata hamasa na mafunzo yatakayosaidia maendeleo ya michezo katika maeneo yao.

Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yameandaliwa na Paul Daud Augustino maarufu MC NIACHEKONA kwa ufadhili wa Shirika la Lushu Foundation, yakilenga kuibua vipaji vya vijana, kukuza michezo na kuimarisha mshikamano wa jamii.

Kwa huduma za MC, matangazo na ushereheshaji wa matukio mbalimbali, wasiliana na MC NIACHEKONA kupitia namba 0757 267 738.

MC NIACHEKONA , akizungumza na watanzania kupitia Misalaba Media.

 SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment

Previous Post Next Post