" UFUKUNYUNGU FC YA SHINYANGA MJINI YATINGA ROBO FAINALI NIACHEKONA CUP BAADA YA KUIONDOA HOME BOYS KWA PENATI

UFUKUNYUNGU FC YA SHINYANGA MJINI YATINGA ROBO FAINALI NIACHEKONA CUP BAADA YA KUIONDOA HOME BOYS KWA PENATI

Na Mapuli Kitina Misalaba


Timu ya Ufukunyungu FC kutoka Kata ya Ngokolo, mjini Shinyanga imefanikiwa kutinga hatua ya robo fainali katika mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 baada ya kuiondoa Home Boys FC ya Kata ya Solwa kwa ushindi wa penati 4-3.

Mchezo huo uliokuwa ukisubiriwa kwa hamu na mashabiki wengi ulimalizika kwa sare ya bila kufungana ndani ya dakika 90 za kawaida, huku timu zote zikishindwa kutumia nafasi walizozipata kutikisa nyavu.

Kutokana na sare hiyo, mshindi alitafutwa kwa mikwaju ya penati ambapo Ufukunyungu FC ilionesha utulivu mkubwa na kufanikiwa kupata penati nne dhidi ya tatu za Home Boys FC.

Ushindi huo umeifanya Ufukunyungu FC kusonga mbele katika hatua inayofuata ya mashindano hayo huku ukiihitimisha safari ya Home Boys FC, timu ambayo ilikuwa ikipewa nafasi kubwa na mashabiki wengi wa Solwa kufika mbali katika mashindano hayo.

Akizungumza baada ya mchezo huo, Katibu wa Kamati ya Mashindano ya NIACHEKONA CUP, Sambayi Jilya, ametangaza ratiba ya mchezo wa kesho ambapo Nyandolwa FC itamenyana na Shilabela FC katika pambano linalotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa huku kila timu ikisaka nafasi ya kusonga mbele.

Sambayi Jilya amewahimiza wananchi, wadau wa michezo na mashabiki kuendelea kujitokeza kwa wingi katika Uwanja wa Mwabenda ili kushuhudia michezo mbalimbali inayoendelea kuibua vipaji vya vijana kupitia mashindano hayo.

Mashindano ya NIACHEKONA CUP 2026 yameandaliwa na Bwana Paul Daud Augustino maarufu MC NIACHEKONA kwa ufadhili wa Shirika la Lushu Foundation, yakiwa na lengo la kuibua vipaji vya vijana, kukuza michezo, kuimarisha mshikamano wa jamii pamoja na kuendelea kudumisha amani kupitia michezo.

Kwa mawasiliano ya shughuli mbalimbali za kijamii, michezo, matangazo na ushereheshaji wa matukio, wasiliana na MC NIACHEKONA kupitia namba 0757 267 738.

Kikosi cha Ufukunyungu FCKikosi cha Home Boys FC.

Post a Comment

Previous Post Next Post