MZEE BOAZ AZIKWA LEO SHINYANGA
Mazishi ya Mzee Boaz Daud Tungu, aliyefahamika na
wengi kwa kujichimbia kaburi lake zaidi ya miaka nane kabla ya kufariki dunia,
yamefanyika leo Agosti 2, 2026 katika Mtaa wa Ndembezi, Halmashauri ya Manispaa
ya Shinyanga.
Akisoma historia ya maisha ya marehemu wakati wa ibada
ya mazishi, mjukuu wake, Bi. Iline Edward, amesema Mzee Boaz alizaliwa Aprili
13, 1929 katika Kijiji cha Nyandekwa Busiya, Wilaya ya Kishapu, mkoani
Shinyanga.
Amesema marehemu alikuwa akisumbuliwa na tatizo la
moyo na kwamba Julai 30, 2026 majira ya saa Nane usiku alifariki dunia akiwa na
umri wa miaka 97.
Kwa mujibu wa historia hiyo, Mzee Boaz ameacha watoto
24, wajukuu 122, vitukuu 139 pamoja na vilembwe watano, huku akiacha kumbukumbu
ya maisha yenye mafundisho na upendo kwa familia yake.
Akizungumza kwa niaba ya familia, mtoto wa nne wa
marehemu, Robert Boaz, ambaye aliwahi kulitumikia Jeshi la Polisi Tanzania
katika nafasi mbalimbali za uongozi, ikiwemo Kamanda wa Polisi katika mikoa
kadhaa na baadaye Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) nchini,
amewashukuru ndugu, jamaa, marafiki na wananchi wote walioshiriki katika
kipindi chote cha kuuguza, kuomboleza na hatimaye kumpumzisha baba yao.
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254
Post a Comment