" WAZIRI MKUU AWASILI TANGA, MGENI RASMI KILELE CHA WIKI YA ELIMU, UJUZI NA UBUNIFU

WAZIRI MKUU AWASILI TANGA, MGENI RASMI KILELE CHA WIKI YA ELIMU, UJUZI NA UBUNIFU

 WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, amewasili leo Jumatatu, Agosti 24, 2026, katika Uwanja wa Ndege wa Mkoa wa Tanga, ambapo anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yanayofanyika katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara, mkoani Tanga.

Amepokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Batilda Burian, pamoja na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Prof. Adolf Mkenda.

Alipowasili katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara, Waziri Mkuu ametembelea mabanda mbalimbali ya maonesho na kujionea bunifu, teknolojia na kazi mbalimbali zinazowasilishwa na washiriki katika maadhimisho hayo.        

SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

  • Wasiliana nasi:
    📍 East African Spirits (T) Ltd
    📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

 




Post a Comment

Previous Post Next Post