Na Mapuli Kitina Misalaba
Mwenge wa
Uhuru umezindua rasmi Tawi jipya la Benki ya CRDB Tinde, mkoani Shinyanga,
katika hatua inayolenga kusogeza huduma za kifedha karibu zaidi na wananchi wa
Tinde na maeneo jirani.
Tawi hilo
lililopo Njiapanda ya Tinde Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, takribani
kilomita 35 kutoka Shinyanga Mjini, limezinduliwa leo Alhamisi, Agosti 20,
2026, ikiwa ni sehemu ya jitihada za CRDB kuongeza upatikanaji wa huduma za
kibenki katika maeneo mbalimbali nchini.
Kiongozi wa
Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Michael Mwang’onda, ameipongeza CRDB kwa
kuendelea kupanua wigo wa huduma za kifedha na kuwekeza katika miundombinu
inayowarahisishia wananchi kupata huduma hizo bila kulazimika kusafiri umbali
mrefu.
Mwang’onda
pia amepongeza ushirikiano kati ya CRDB na Serikali katika utekelezaji wa
programu mbalimbali za kuwawezesha wananchi kiuchumi, ikiwemo utoaji wa mikopo
kwa makundi mbalimbali pamoja na kushiriki katika shughuli za kijamii na
michezo.
Kwa upande
wake, Mkurugenzi wa Mikopo wa CRDB, Xavery Makwi, akimwakilisha Mkurugenzi
Mtendaji wa benki hiyo, Dkt. Abdulmajid Mussa Nsekela, amesema uwepo wa tawi
hilo Tinde utasaidia kupunguza changamoto ya wananchi kusafiri hadi Shinyanga
Mjini kwa ajili ya kupata huduma za kibenki.
Makwi
amesema CRDB tayari imetoa mikopo yenye thamani ya shilingi trilioni 31 kwa
makundi mbalimbali, wakiwemo wakulima, wafanyabiashara, watumishi, wastaafu na
watu binafsi, huku akiwataka wananchi wa Tinde kutumia fursa zinazotolewa na
benki hiyo kuimarisha shughuli zao za kiuchumi.
Tawi la CRDB
Tinde ni miongoni mwa matawi 25 ya benki hiyo katika Kanda ya Magharibi,
inayohusisha mikoa ya Shinyanga, Tabora, Kigoma na Geita.
Ujenzi wa
jengo hilo jipya ulianza mwaka 2016 na umehusisha uwekezaji wa shilingi milioni
650, zilizotumika katika ununuzi wa eneo, ujenzi wa jengo pamoja na uwekaji wa
vifaa muhimu vya huduma za kibenki. Tawi hilo lilianza kutumia jengo hilo jipya
mwezi Aprili 2026.
Taarifa za
maendeleo ya huduma za tawi hilo zinaonesha kuwa tayari zaidi ya wananchi
10,000 wamefungua akaunti za benki kupitia Tawi la CRDB Tinde, jambo
linaloashiria ongezeko la matumizi ya huduma rasmi za kifedha katika eneo hilo.
Baadhi ya wananchi
wa Tinde na maeneo jirani wameipongeza CRDB kwa kusogeza huduma hizo karibu
nao, wakieleza kuwa hatua hiyo imepunguza gharama na muda ambao walikuwa
wakitumia kusafiri hadi Shinyanga Mjini kwa ajili ya huduma kama kuweka na
kutoa fedha.
Uwepo wa
tawi hilo pia unatarajiwa kuongeza fursa kwa wananchi kupata huduma za kifedha
kwa urahisi zaidi na kuchochea ukuaji wa shughuli za biashara na uchumi wa kaya
katika Tinde na maeneo yanayolizunguka.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Michael Mwang’onda, akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Tawi la CRDB Tinde.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Michael Mwang’onda, akizungumza wakati wa uzinduzi wa Tawi la CRDB Tinde mkoani Shinyanga.
Mkurugenzi wa Mikopo wa Benki ya CRDB, Xavery Makwi, akikabidhi taarifa ya mradi huo.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Michael Mwang’onda, akitembelea na kukagua jengo jipya la Tawi la CRDB Tinde, Shinyanga.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Michael Mwang’onda, akisaini kitabu cha wageni kwenye Tawi la CRDB Tinde, Shinyanga.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Michael Mwang’onda, akiwa katika zoezi la kufungua jiwe la msingi la jengo jipya la Tawi la CRDB Tinde.
Mkurugenzi wa Mikopo wa Benki ya CRDB, Xavery Makwi, akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Tawi la CRDB Tinde mkoani Shinyanga.
Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi Jumanne Wagana, akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Tawi la CRDB Tinde mkoani Shinyanga.
Meneja wa CRDB tawi la Tinde akizungumza.




SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254














































Post a Comment