Inaelezwa kuwa tukio hilo lilitokea baada ya watu kufika kumchukua ng’ombe huyo nyumbani kwa mzee Mzee Monisa, ambaye alikua mfugaji kwa ajili ya kwenda kumpandisha jike.
Inadaiwa
kuwa walipomfikia, ng’ombe huyo alikimbia na kufika katika eneo la jirani,
anakoishi Mzee Monisa.
Mzee
Monisa alichukua fimbo na kujaribu kumrudisha ng’ombe huyo, lakini ng’ombe huyo
alimgeukia na kumkanyaga.
Baada
ya tukio hilo, Mzee Monisa alikimbizwa katika Hospitali ya Manispaa ya
Shinyanga kwa ajili ya matibabu.
Inadaiwa
kuwa baada ya kufanyiwa vipimo, ilibainika kuwa alikuwa amevunjika mbavu,
lakini alifariki dunia akiwa anapatiwa matibabu.
Mzee
Monisa alikuwa mfugaji,
na hadi umauti ulipomkuta alikuwa akihudumu kama Mwenyekiti wa CHADEMA Kata ya Ngokolo.
Pia,
Mzee Monisa aliwahi kuwa Mwenyekiti
wa Serikali ya Mtaa wa Mwinamila, Kata ya Ngokolo, Manispaa ya Shinyanga.
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

Post a Comment