" ASKOFU SANGU AENDELEA KUSHUHUDIA MOYO WA IMANI NA MAJITOLEO YA WAAMINI KWA KANISA, AIMARISHA WAKRISTO WAPYA 1,252

ASKOFU SANGU AENDELEA KUSHUHUDIA MOYO WA IMANI NA MAJITOLEO YA WAAMINI KWA KANISA, AIMARISHA WAKRISTO WAPYA 1,252


 Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu, ameendelea kushuhudia matunda ya moyo wa imani na majitoleo kwa Kanisa kutoka kwa Waamini, kupitia ziara ya kichungaji aliyoifanya hivi karibuni katika Parokia tatu za Mwamapalala Wilayani Itilima mkoani Simiyu, Mwandoya wilayani Meatu mkoani Simiyu na Maganzo wilayani Kishapu mkoani Shinyanga.

Kupitia ziara hiyo, Askofu Sangu ametoa Sakramenti ya Kipaimara kwa idadi kubwa ya Wakristo wapya, wakubwa kwa wadogo, inayofikia watu 1,252, ambapo kati ya hao, 660 ni wa Parokia moja ya Mwamapalala , 450 ni wa Parokia ya Mwandoya na 142, ni wa Parokia ya Maganzo.

Pia, amebariki na kuzindua makanisa mapya mawili pamoja na Groto kwa ajili ya heshima kwa Mama Bikra Maria, kwenye vigango vya Ngh’omango na Mwalushu vilivyopo katika Parokia ya Mwamapalala, vilivyojengwa kwa nguvu za waamini kwa kushirikiana na wasamaria wema.

Halikadhalika, amefungua ukumbi mpya pamoja na kuweka jiwe la msingi katika jengo la utawala na maabara ya kisasa linaloendelea kujengwa katika shule ya Sekondari Mwamapalala, inayomilikiwa na Kanisa Katoliki Jimbo la Shinyanga.

Kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki Jimbo la Shinyanga, pamoja na kuwapongeza Waamini kwa namna ambavyo wametambua umuhimu wa kujitoa kwa ajili ya ustawi wa Kanisa lao, ameendelea kuwasisitiza kuwa na moyo wa imani na majitoleo kwa Kanisa , ambalo kwa sasa halitegemei tena misaada kutoka nje ya nchi kama ilivyokuwa hapo awali, na badala yake kazi ya umisionari imeachwa mikononi mwa Waafrika wenyewe.

Askofu Sangu pia ametumia nafasi hiyo kupeleka ujumbe wa amani na upendo kwa watu wote, huku akiwataka Wakristo kuwa na hofu ya Mungu kwa mambo yote wanayoyafanya, hali ambayo ameitaja kuwa itawawezesha kuepuka kushiriki katika matendo maovu yanayomchukiza mwenyezi Mungu, ambayo ni pamoja na kuziona shida za wengine kama fursa ya kujipatia kipato badala ya kuwasaidia, na kuwa chanzo cha chuki na mafarakano miongoni mwa jamii.

MATUKIO MBALIMBALI KATIKA PAROKIA YA MWAMAPALALA

Mapokezi ya Askofu Sangu katika Parokia ya Mwamapalala
Askofu Sangu akisalimiana na baadhi ya Waamini wa Parokia ya Mwamapalala mara baada ya kuwasili katika Parokia hiyo
Askofu Sangu akizindua Kanisa la Kristo Mfalme Kigango cha Ngh’omango
Askofu Sangu akifungua Groto ya Mama Bikra Maria katika Kigango cha Ngh’omango
Askofu Sangu akitoa heshima kwa Mama Bikra Maria baada ya kufungua Groto
Muonekano wa nje wa Kanisa la Kristo Mfalme Kigango cha Ngh’omango
Askofu Sangu akiwa ndani ya Kanisa la Kristo Mfalme baada ya kulifungua rasmi
Kanisa jipya la Kigango cha Mwalushu
Muonekano wa ndani wa Kanisa la Kigango cha Mwalushu

Askofu Sangu akiongoza sala kwa heshima ya Mama Bikra Maria mara baada ya kuzindua Kanisa na Groto katika Kigango cha Mwalushu
Askofu Sangu akipokelewa na wanafunzi katika shule ya Sekondari Mwamapalala
Askofu Sangu akikata utepe kuzindua ukumbi wa shule

Askofu Sangu akiweka jiwe la msingi katika ujenzi wa jengo la utawala na maabara ya kisasa katika shule ya Sekondari Mwamapalala
Askofu Sangu akisaini kitabu cha wageni katika shule ya Sekondari Mwamapalala, kulia ni mkuu wa shule hiyo Padre Joseph Komanya na wa pili kushoto ni Paroko wa Parokia ya Mwamapalala Padre Beatus Maduhu
Askofu Sangu akiagana na baadhi ya wanafunzi wa shule ya Sekondari Mwamapalala mara baada ya kutembelea shule hiyo kama sehemu ya ziara yake katika Parokia ya Mwamapalala
Askofu Sangu akiongoza Misa takatifu ya Kipaimara katika siku ya pili ya ziara yake katika Parokia ya Mwamapalala
Askofu Sangu akitoa Sakramenti ya Kipaimara katika Parokia ya Mwamapalala
Askofu Sangu akiendelea na adhimisho la Misa takatifu katika Parokia ya Mwamapalala, aliyeshika Mic ni Paroko msaidizi wa Parokia hiyo na mkuu wa shule ya Sekondari Mwamapalala Padre Joseph Komanya, wa kwanza kushoto ni Padre Paslay Marwa kutoka jimbo la Musoma na wa pili kushoto ni Paroko wa Parokia hiyo padre Beatus Maduhu
Askofu Sangu akiwakomunisha waimarishwa katika Parokia ya Mwampalala
Baadhi ya waamini wa Parokia ya Mwamapalala ikiwemo waimarishwa wakiwa katika adhimisho la Misa takatifu ya Kipaimara

Wanakwaya wa Parokia ya Mwamapalala na utoto mtakatifu wa Yesu wakiwa katika adhimisho la Misa takatifu

Waimarishwa na waamini wakimtolea Mungu shukrani

Askofu Sangu akikabidhi cheti cha pongezi kwa baadhi ya wanandoa ambao wamedumu kwa zaidi ya miaka 25

MATUKIO MBALIMBALI KATIKA PAROKIA YA MWANDOYA

Fratel Boniphace Seleka kutoka Parokia teule ya Lagangabilili akisoma somo la pili katika Misa ya Kipaimara iliyofanyika katika Parokia ya Mwandoya
Padre Prasad George (SMA) akisoma somo la Injili
Askofu Sangu akitoa Homilia kwenye Misa ya Kipaimara katika Parokia ya Mwandoya

Askofu Sangu kwa kushirikiana na Mapadre wa Parokia ya Mwandoya akiongoza sala maalum ya kwa ajili ya kuwaimarisha Waimarishwa
Askofu Sangu akitoa Sakramenti ya Kipaimara katika Parokia ya Mwandoya

Makatekista wa Parokia ya Mwandoya wakiwa kwenye Misa ya Kipaimara
Askofu Sangu kwa kushirikiana na Mapadre wa Parokia ya Mwandoya akiendelea na adhimisho la Misa takatifu

Paroko msaidizi wa Parokia ya Mwandoaya Padre Michael Mick (SMA) akimkomnisha mmoja wa Waamini waliohudhuria Misa

Paroko wa Parokia ya Mwandoya Padre Marek Krysa (SMA) akiwakomunisha Waamini

Padre Prasad George (SMA) akiwakomunisha Waamini

Askofu Sangu akiwakomunisha Waimrishwa

Paroko wa Parokia ya Mwandoya Padre Marek Krysa (SMA) akitoa neno la shukrani kwa Mhashamu Baba Askofu

Utoto mtakatifu wa Yesu Parokia ya Mwandoya katika picha ya pamoja na Mhashamu Baba Askofu Sangu

Paroko msaidizi wa Parokia ya Mwandoaya Padre Michael Mick (SMA) akitoa neno la shukrani

Askofu Sangu akizungumza na Waamini wa Parokia ya Mwandoya mara baada ya Misa na kuwashukuru kwa moyo wa imani na jitihada zao za kulitegemeza Kanisa

MATUKIO MBALIMBALI KATIKA PAROKIA YA MAGANZO

Mapokezi ya Askofu Sangu katika Kigango cha Idukilo Parokia ya Maganzo

Paroko wa Parokia ya Maganzo Padre Emmanuel Kahabi akimkaribisha Askofu Sangu katika kigango cha Idukilo

Askofu Sangu akibariki na kuzindua Tabernakulo (chombo maalum cha kuhifadhia mwili na damu ya Kristo) katika Kigango cha Idukilo
Paroko wa parokia ya Maganzo Padre Emmanuel Kahabi akimkaribisha Mhashamu Baba Askofu kwa ajili ya adhimisho la Misa takatifu ya Kipaimara

Askofu Sangu akitoa Homilia katika Misa ya Kipaimara

This image has an empty alt attribute; its file name is 178A0693-1024x683.jpg
Katibu wa Askofu Padre Deusdedith Kisumo akimkaribisha Paroko wa Parokia ya Maganzo kuwatambulisha Waimarishwa kwa Askofu
Paroko wa parokia ya Maganzo Padre Emmanuel Kahabi akiwatambulisha Waimarishwa kwa Askofu
Askofu Sangu kwa kushirikiana na Mapadre akiongoza sala maalum ya kuwaimarisha Waimarishwa
Askofu Sangu akitoa Sakramenti ya Kipaimara katika Parokia ya Maganzo
Askofu Sangu akipokea matoleo katika Parokia ya Maganzo
Waimarishwa wa Parokia ya Maganzo wakipeleka matoleo yao
Wanakwaya wa Parokia ya Maganzo wakiwa katika Misa
Askofu Sangu akiwakomunisha Waimarishwa katika Parokia ya Maganzo
Katibu wa Askofu Padre Deusdedith Kisumo akiwakomunisha waamini

Paroko wa parokia ya Maganzo Padre Emmanuel Kahabi akiwakomunisha wanakwaya
Askofu Sangu akiwa na Paroko wa Parokia ya Maganzo Padre Emmanuel Kahabi
Askofu Sangu aktika Picha ya pamoja na makundi mbalimbali Parokiani Maganzo
Askofu Sangu akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Waimarishwa katika Parokia ya Maganzo
Paroko wa Parokia ya Maganzo Padre Emmanuel Kahabi akitoa neno la shukrani kwa Askofu
Baadhi ya waamini wa Parokia ya Maganzo wakiwa kwenye eneo la Misa
Picha ya pamoja na wawakilishi wa makundi mbalimbali ndani ya Kanisa

Post a Comment

Previous Post Next Post