" KINACHOENDELEA UJENZI WA KITUO CHA MABASI MJINI BUKOBA

KINACHOENDELEA UJENZI WA KITUO CHA MABASI MJINI BUKOBA

 



Na Fabius Clavery ,Misalaba BLOG-KAGERA

Mkuu wa mkoa wa Kagera mhe.Albert Chalamila amesema  kuwa licha  ya wazo la ujenzi wa kituo  kubwa cha mabasi mjini Bukoba (BUKOBA BUS TERMINAL) kuanzishwa katika kata ya Nyanga eneo la Kyakailabwa  bado mkoa huo unaangalia kama  eneo hilo linafaa kwa ajili ya ujenzi huo kuendelezwa ama kuhamishiwa katika eneo jingine.

Mhe.Chalamila aliyasema hayo   November 12,2022 wakati akieleza vipaumbele vya mkoa huo kwa waandishi wa habari ambapo alisema suala la stendi serikali ya mkoa huo inaangalia kama eneo la kwanza linafaa au kuna haja ya kutafta eneo jipya .

“nyinyi mtakumbuka kwamba sitendi sasa inatengenezwa pale Kyakailabwa na tayari kuna ile bilioni moja iliyokwisha ahidiwa kwa ajili ya kuanza maandalizi ya ujenzi .Swali la msingi ni kwamba  leo hii tumeanza maandalizi ya kutengeneza stendi yetu ya Kyakailabwa lakini swali kubwa ambalo wadau lazima tuwashirikishe vizuri je, kati ya njia kutoka Mutukula kuingia hapa kwetu Bukoba na kati ya njia kutoka Muleba  kuingia hapa kwetu ni ipi ina magari mengi? Kwaio majibu yawezekana badae mkaja kuniambia kwamba inawezekana hii ya Muleba ikawa na magari mengi. Na kwamantiki hiyo bado tunashirikisha zaidi pia watalamu kwamba pesa kubwa hiyo itakapo kuwa imepatikana tuone je kuna haja ya kuendeleza wazo lile la ujenzi wa stendi Kyakailabwa au tuweze kuiweka somewhere unapokaribia kuingia mjini kwa upande unapotoka Muleba sasa hilo litakuwa ni swala mtambuka ambalo tutawakaribisha pia wadau liweze kuwa ni suala la pamoja ili tuone kwamba sasa tusikaribishe mzunguko ambao utakuwa hauna maana kwa wananchi wetu ” alifafanua Chalamila mkuu wa mkoa huo.

 

Aliyewahi kuwa Meya wa manispaa ya Bukoba mkoani Kagera bw,Chief Andronicus Karumuna alikiambia kituo hiki kuwa  baraza la madiwani  mwaka 2015-2020 liliamua kuanzisha wazo la ujenzi wa kituo hicho cha mabasi nje kidogo ya mji katika eneo la Kyakailabwa kwalengo wa kupanua mji huo na  kodi za watanzania zaidi ya milioni 800 zilikwishatumika katika utekelezaji wa mradi huo ambao awakufanikisha kuukamilisha kutokana na sababu za kifedha.

“Pindi tulipounda baraza letu tulikuwa namipango mbalimbali lakini kubwa zaidi tulikuwa naishu ya utengenezaji wa stendi kwamaana ya kuhamisha stendi kutoka hapa ilipo na kuijenga katika maeneo ya Kyakailabwa katika manispaa ya mji wa Bukoba katika kata ya Nyanga na tulifanya mambo yafuatayo ya msingi, kwanza kile kiwanja ambacho kilitakiwa kitumike  kwa ajili ya masuala ya ujenzi wa stendi ilikuwa ni ardhi iliyomilikiwa nawananchi mbalimbali wa mji wa Bukoba kwaio  swala la kwanza ilikuwa ni kutafuta fedha ambazo zilitakiwa kwenda kufanya fidia, tulitafta hizo fedha na tukawalipa watu waliokuwa wanamiliki hilo eneo kwa ajili ya kupisha ujenzi ” alieleza chief karumuna aliyewahi kuwa meya wa manispaa ya Bukoba.

“kupitia fedha za ndani tuliweza kuengeneza yafuatayo, kwanza Barabara zinzozunguka stendi ya Kyakailabwa ni takribani mita 800  kwaio katika uongozi wetu tuliacha tumejenga mita 400 kwa kiwango cha lami kati ya mita 800 zinazozunguka kiwanja lakini pili hatukuwa na maji pale tulipata bahati ya kuweka maji  katika eneo lile, hakukuwa na umeme  tulibahatika kuweka umeme hatukuwa navyoo tukajenga vyoo Me na Ke, lakini pia tukajenga jengo la polisi ambalo kimsingi tuliacha limekamilika, lakini pia tukajenga waiting-shave tatu  kwa ajili ya abiria pamoja na kuweka parking kwa ajili ya malori na magari mengine na ninafikiri tutakuwa tumewekeza takribani milioni kama 900  hivi na ushee” aliongeza Chief Karumuna.

Kadhalika Bwana Karumuna  anashauri kuwa ni vyema mpango huo undelezwe  na kukamilishwa kwa ajili ya manufaa ya wananchi wa mkoa wa Kagera.

Wilifred Rwakatale  aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Bukoba mjini anasema kuhama kwa kituo hichokutoka kilipo kwa sasa  ni muhimu  na eneo lililopendekezwa linafaa zaidi kwani  ni eneo ambalo kwa jiografia ya manispaa ya Bukoba ndilo eneo ambalo alijaendelezwa na litakuwa na fursa kwa wakazi wa Bukoba na Kagera kwa ujumla.

“huo mpango sio waleo wala jana wala juzi kwaio tunatarajia waliopo madarakani watakamilisha huo mpango mji wa Bukoba jinsi ulivyo kiramani hiyo stendi ingewaza kusaidia kupanua mji kwa jinsi ilivyo kwa msingi kwamba hilo eneo ambalo walipanga liwe stendi liko nje kidogo ya mji wa sasa na hilo eneo waliloweza kuposition liko wazi  na linapakana na maeneo mengine ambayo ni makubwa yaliyoko nje ya Bukoba”Alisema Rwakatale aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Bukoba mjini.

 

Bwana William Osward Rutta mkurugenzi wa kampuni ya utalii ya Bukoba Tours iliyopo mjini Bukoba anasema kuwa stendi ni fursa kubwa ya biashara na uchumi hivyo inafaa mchakato wa ujenzi wa kituo cha mabasi cha mji huo ukashughulikiwa haraka kutokana na mkoa wa Kagera kupakana na mataifa jirani kama Uganda Rwanda na Burundi ,anaongeza  kuwa  hata stendi iliyopo hivi sasa miundombinu yake sio rafiki   ukilinganisha na vituo vya mabasi vilivyopo katika mikoa  mingine  hapa nchini.

“stendi ni fursa kubwa ya biashara na kiuchumi katika sehemu yoyote ,wakati nikiwa nasafiri huwa sipendi kushuka katika sitendi hiyo maana ni majanga matupu ,lakini kwa sababu wamekwisha sema ipo Billion moja  kwa mkandarasi sio hela ndogo ,basi hiyo miundombinu iendelee kuwekwa . saa hizi ukifika Chato unafurahi sana stendi ya magari madogo na makubwa inafurahisha  sana  lakini ukienda Kigoma hata stendi ya katikati ya mji unakuwa kama uko Ulaya yaani Kigoma panavutia kweli ukienda stendi kubwa ni nzuri ukienda stendi nyingine ukienda  morogoro ukienda Dodoma kwakweli unaona nisehemu ambapo  mtu unaweza ukaenda kutalii.Kwaio ni nafasi kubwa hatujachelewa  ingawa tumechelewa  kuhakikisha na sisi tunakuwa na stendi ya kisasa yenye kukidhi mahitaji ya Tanzania na wageni wanaotoka nchi za nje wanaokuja kutembelea mkoa wa Kagera  ”alieleza bwana Osward Rutta

Mchambuzi wa masuala mbalimbali nchini Tanzania  bwana Hamuduni Maliseli Anatoa rai kwa wataalamu waliopo ofisini katika manispaa ya Bukoba kushirikiana na wataalamu wazawa  ndani ya mkoa huo  walioko mikoa Mbalimbali  na maeneo tofauti  ulimwenguni kujenga mji huo kisasa.

“Wamekwenda mahara wamekwenda Uswisi wamekwenda Marekani wamekwenda Uingereza wamekwenda Ufaransa na  Ujerumani wamekwenda Italia wameona watu wanavyojenga miji inavyopangwa na kadhalika ,kwaio mimi nafikiri jambo hili linatia aibu kubwa  sana kwakweli na hasa linapotikea kwa mji kama bukoba kwa nchi ya watu aliofanikiwa kupiga hatua ya kimaendeleo na kifikra mapema” alieleza bwana Hamuduni

“na wale wanaokwenda Kagera viongozi kutoka mikoa mingine wasipaone kwamba haa! wacha pawe hivyo kwa sababu sio kwetu hapana! huko ulipokwenda ndo kwenu na sifa utakayoipata  ni kule ulikofanyia kazi sio kule ulikozaliwa kwaio mimi nafikiri ni muhimu sana kwa viongozi wa sasa”aliongeza Hamuduni

Hamad Isimaili Hamisi ni mmoja ya madereva wanaotumia kituo cha mabasi cha Bukoba anasema hali ya kituo hicho huwa mbaya zaidi hasa katika kipindi cha mvua lakini anaongeza kuwa kituo hicho kina eneo dogo ambalo upelekea kufanya kazi zao kwa mazingira magumu kwani wakati mwingine magari hukosa nafasi zakuingia na kutoka.

“changamoto kwanza tope yaani tope linatukera alafu stendi hii inabana  tunataka angalau tuwe na stendi mbili angalau aice na kosta zijumuike sehemu moja na  mabasi yawe na stendi yake itakuwa ni bora kwani stendi ya kyakailabwa ikiwepo nahii ikawepo iashara itakwenda vizuri hata hapa stendi kelele zitapungua na hizi stendi zinatakiwa zisakafiwe  zifanane na mikoa mingine hapa hakuna hata sehemu ya abiria kusubiri gari unakuta wakati mwingine wamo wanarandaranda humu ikitokea patroo ya polisi  abiria anakamatwa kama mwizi ni changamoto hakuna utaratibu ” alieleza dereva hamadi Isimaili

Akiwa katika mkutano wa hadhara katika kata ya Nyanga October 27,2022 mbunge wa  jimbo la Bukoba  mjini ambaye pia ni naibu waziri wa Nishati nchini Stephen Byabato alisema kuwa ujenzi wa kituo hicho utaendelezwa muda wowote kwani tayari serikali ilikwisha idhinisha billion moja kwa ajili ya shughuli hiyo.

“hapa tulipo ni eneo la stendi ya mabasi ya Bukoba mjini hakuna maneno mengi mama samia alishatuhaidi atatujengea stendi  mweshimiwa makamu wa Rais alipokuja  mwezi wanne alileta ahadi ya mweshimiwa Rais Smia na tulivyobembeleza akasema kwa kuanzia atatupatia shilingi bilioni moja kwa ajili ya kuanzia maendeleo ya  stendi yetu ndugu zangu wananyanga hili ni eneo la stendi nay ale maswali yalikuwa yanaulizwa stendi itajengwa lini itajengwa lini stendi itaanza kujengwa muda sio mrefu kwa sasabu tayari mama samia amekwisha tuahidi billion moja,mradi wa stendi huu ulikuwa na vitu vinne ndani yake  niwambie vitu vingine labda ambavyo hamvijuhi eneo hili la stendi limetengwa kwa ajili ya vitu vinne kuna gereji hapa kuna stendi ya magari madogo kuna stendi ya magari makubwa sehemu ya kuegesha malori kwaio kuna miradi minne ndani ya mradi mmoja.”

Ikumbukwe  kuwa mnamo Juni 9 2022,Rais wa jamhuri wa muungano wa Tanzania mhe.Samia Suluhu Hassan  Wakati akihutubia wananchi wa mkoa wa kagera katika uwanja wa kaitaba alipokuwa ziarani mkoani humo alisema“lakini mahitaji mengine mliyonayo hapa kama alivyosema mbunge wa bukoba mjini ni soko la kisasa na stendi ya kisasahabari njema ni kwamba katika mwaka wa fedha 2022/2023 serikali imetenga jumla ya shilingi billion moja kwa ajili ya kuanza ujenzi wa stendi ya kisasa lakini pamoja na fedha hiyo kuna  mradi unaofadhiliwa na benki ya dunia kwa lengo la kuboresha miundombinu ya miji unaojulikana kama TACTIC kama alivyosema mweshimiwa mbunge,mradi huu utakapoanza kutekelezwa mbali na kufadhili ujenzi wa stendi ya kisasa utafadhili pia ujenzi wasoko kuu la manispaa ya bukoba”

Mkuu wa mkoa wa Kagera mhe.Albert Chalamila





 

Post a Comment

Previous Post Next Post