Na Mapuli Misalaba, Shinyanga
Afisa ustawi wa jamii Mkoa wa Shinyanga Lydia Kwesigabo
ametoa maagizo mbalimbali kwa viongozi
wanao tekeleza kampeni ya shujaa wa maendeleo na ustawi wa jamii Tanzania
SMAUJATA Mkoa wa Shinyanga.
Maelekezo hayo ni pamoja na kufanya kazi kwa weledi,
kutoa taarifa kwa vyombo husika kama polisi na ofisi za ustawi wa jamii pale
wanapobaini au kupewa taarifa kuwa kunatukio la ukatili wa kijinsia au ukatili
wa mtoto.
Ametoa maagizo hayo katika kikao cha pamoja cha
viongozi wa serikali na viongozi wa vyuo wa SMAUJATA Mkoa wa Shinyanga ambapo pamoja
na mambo mengine Lydia amewasisitiza kushirikiana kwa pamoja katika utekelezaji
wa majukumu ya kupinga ukatili.
Kwa upande wao baadhi ya viongozi wa SMAUJATA Mkoa
wa Shinyanga waliohudhuria kikao hicho wameahidi kuendelea kushirikiana na
kwamba watazingatia maelekezo yote yanayotolewa na viongozi wa serikali.
Aidha katika kikao hicho mratibu wa elimu ya afya
kwa umma Dkt. Moses Mwita ametumia nafasi hiyo kutoa elimu juu ya kujikinga na magonjwa
ya kuambukiza.
“Kila
mmoja ahakikishe swala linalohusu afya alipe kipaumbele kuliko kitu chochote
kwa mfano mimi hapa nimempenda binti lakini ninatakiwa nijepe kipaumbele kwamba
nitapima naye kwanza ndiyo tufanya chochote tunachotaka kufanya yaani katika
hili tukiweza kufanya hivi sisi sote tukaweza kujizuia kabla ya kufanya
tutasaidia watoto”.
“Hayo
nayasema nikiwa na maana ya kwamba tukifanikiwa kuacha ngono ndiyo tunaweza
kupunguza maabukizi ya magonjwa yaani kila mmoja anapaswa kuwa na msimamo kwenye
nafasi yake na ninatamani sana tubadilike katika hilo hasa sisi vijana ukitaka
kuingia kwenye mahusiano ya kimapenzi na mtu nenda kapime chukua hatua zote ili
awe salama na wewe ubaki kuwa salama kwa sababu haya mambo bado yanaendelea
kwenye jamii yetu na ndiyo maana maabukizi ya majowa yanaongezeka”. Amesema
Dkt. Mwita
AFISA USTAWI WA JAMII LYDIA ATOA MAAGIZO KWA SMAUJATA MKOA WA SHINYANGA
Na Mapuli Misalaba, Shinyanga
Afisa ustawi wa jamii Mkoa wa Shinyanga Lydia Kwesigabo
ametoa maagizo mbalimbali kwa viongozi
wanao tekeleza kampeni ya shujaa wa maendeleo na ustawi wa jamii Tanzania
SMAUJATA Mkoa wa Shinyanga.
Maelekezo hayo ni pamoja na kufanya kazi kwa weledi,
kutoa taarifa kwa vyombo husika kama polisi na ofisi za ustawi wa jamii pale
wanapobaini au kupewa taarifa kuwa kunatukio la ukatili wa kijinsia au ukatili
wa mtoto.
Ametoa maagizo hayo katika kikao cha pamoja cha
viongozi wa serikali na viongozi wa vyuo wa SMAUJATA Mkoa wa Shinyanga ambapo pamoja
na mambo mengine Lydia amewasisitiza kushirikiana kwa pamoja katika utekelezaji
wa majukumu ya kupinga ukatili.
Kwa upande wao baadhi ya viongozi wa SMAUJATA Mkoa
wa Shinyanga waliohudhuria kikao hicho wameahidi kuendelea kushirikiana na
kwamba watazingatia maelekezo yote yanayotolewa na viongozi wa serikali.
Aidha katika kikao hicho mratibu wa elimu ya afya
kwa umma Dkt. Moses Mwita ametumia nafasi hiyo kutoa elimu juu ya kujikinga na magonjwa
ya kuambukiza.
“Kila
mmoja ahakikishe swala linalohusu afya alipe kipaumbele kuliko kitu chochote
kwa mfano mimi hapa nimempenda binti lakini ninatakiwa nijepe kipaumbele kwamba
nitapima naye kwanza ndiyo tufanya chochote tunachotaka kufanya yaani katika
hili tukiweza kufanya hivi sisi sote tukaweza kujizuia kabla ya kufanya
tutasaidia watoto”.
“Hayo
nayasema nikiwa na maana ya kwamba tukifanikiwa kuacha ngono ndiyo tunaweza
kupunguza maabukizi ya magonjwa yaani kila mmoja anapaswa kuwa na msimamo kwenye
nafasi yake na ninatamani sana tubadilike katika hilo hasa sisi vijana ukitaka
kuingia kwenye mahusiano ya kimapenzi na mtu nenda kapime chukua hatua zote ili
awe salama na wewe ubaki kuwa salama kwa sababu haya mambo bado yanaendelea
kwenye jamii yetu na ndiyo maana maabukizi ya majowa yanaongezeka”. Amesema
Dkt. Mwita
Afisa ustawi wa jamii Mkoa wa Shinyanga Lydia Kwesigabo
mratibu wa elimu ya afya kwa umma Dkt. Moses Mwita
Katibu wa SMAUJATA Mkoa wa Shinyanga Masunga Dotto akizungumza katika kikao hicho
Post a Comment