" MEYA WA MANISPAA YA SHINYANGA MH: MASUMBUKO AWAPA NONDO ZA MAISHA WAHITIMU CHUO CHA UFUNDI MATANDA VTC

MEYA WA MANISPAA YA SHINYANGA MH: MASUMBUKO AWAPA NONDO ZA MAISHA WAHITIMU CHUO CHA UFUNDI MATANDA VTC


Na Mapuli Misalaba, Shinyanga

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga mheshimiwa Elias Ramadhan Masumbuko amewataka wanafunzi wanaohitimu mafunzo ya ufunzi VETA kutokata tamaa na kwamba wanapaswa kufanya kazi pamoja na kujiajiri kutokana na ujuzi walioupata.

Ameyasema hayo kwenye mahafali ya pili ya chuo cha ufundi stadi Matanda  Vocational Training Centre kilichopo kata ya Chamaguha Manispaa ya Shinyanga ambapo jumla ya wanafunzi 10 wamehitimu mafunzo katika  kozi mbalimbali ikiwemo umeme pamoja na umekanika.

Mheshimiwa Elias Masumbuko ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo amewasisitiza wahitimu kufanya kazi kwa bidii  kujiamini hasa pale wanapokuwa katika shughuli zao za ujunzi waliofundishwa.

Amewakumbusha kujiendeleza zaidi ili kuwa wabobevu wa kitaaluma kwenye ujunzi ambao wamejifunza huku akiwaasa kuondoa dhana mbaya ya kusubiria ajira serikalini na kwamba ujunzi huo wautumie kujiajiri ili kufikia malengo.

“Leo mnahitimu kuna mambo ya kielimu ambayo mmekuwa mkiyapata hapa chuoni cha kwanza mkajiendeleze huu siyo mwisho, ulimwengu wa sasa ni ulimwengu wa kiteknolojia unamambo mengi yanayobadilika kila siku yanahitaji uelewa wa kutoka kwahiyo msilizike sana na kiwango cha mafunzo ambayo mmekuwa mkifundishwa hapa ni vyema sasa mkachukua hatua mkajiendeleza zaidi kutoka hapo mlipo ili kwa badae muwe mafundi, wataalam wabobevu wa kitaaluma kwa taaluma zenu ambazo mmejifunza”.amesema Meya Masumbuko

“Mnatakiwa kujiamini  muondoe ile hofu kile mtakachoenda kukifanya mkifanye kwa kujiamini na siyo kwa kujaribu itakuwa ni busara sana huko muendako kuionyesha heshima hii ambayo mmeondoka nayo hapa kwa wazazi wenu na jamii yote inayowazunguka na kwa muonekano wenu jinsi mnavyojituma, mkifanya kazi kwa  bidii katika utendaji wenu watatamani na wengine kuja VTC Matanda”.

“Mara nyingine vijana wanapoteza ari wanakata tamaa anasoma akifikiri kuwa serikali itamuajiri baada ya kukosa ajira anachoka anakata tamaa anaanza kulaumu hata elimu aliyojifunza kwa nini tunafikia hatua kama hiyo tubadilishe mitazamo yetu sasa kwamba kumbe tunapotoka katika elimu fundisho, elimu taaluma tunapaswa kwenda kufanya kazi ya kujiajiri sisi kutokana na ujunzi tulioupata”.amesema Meya Masumbuko

Aidha mstahiki meya wa Manispaa ya Shinyanga ambaye pia ni Diwani wa kata ya Chamaguha Mh: Elias Masumbuko amesema serikali inatoa fursa mbalimbali ambapo kila mwananchi anapaswa kuchangamkia ikiwemo fursa ya mikopo yenye riba nafuu inayotolewa katika kila Halmashauri kwa kuzingatia kundi la vijana, wanawake pamoja na watu wenye ulemavu.

Kwa upande  mkuu wa chuo cha ufundi stadi Matanda Vocational Training Centre (VTC) Bwana Joaster Thomas Kisanko akisoma taarifa fupi ya chuo ametaja baadha ya mafanikio yaliyopo ikiwemo kujenga na kukarabati madarasa pamoja na bwani.

“Chuo cha matanda VTC kina historia ndefu tangu Mwaka 1989 wakati wa marehemu Castory Sekwa aliyekuwa Askofu wa jimbo katoliki  Shinyanga kwa msaada wa Misereor – Germany”.

“Mnamo Mwaka 2010 chuo kilishindwa kupata sifa za uendeshaji mafunzo kwa mujibu wa VETA – Taifa lakini Mwaka 2018 chuo kilifunguliwa tena na Mhasham Baba Askofu Liberatus Sangu ambaye ni Askofu jimbo katoliki Shinyanga na kuanzishwa fani tano ambazo tunaendelea nazo fani ya Umeme, Umekanika, Ushonaji, Uashi, Uungaji vyuma pamoja na Udereva”.amesema Kisanko

“Sasa hivi chuo pia kinatoa mafunzo ya Kompyuta kwa daraja la pili na kwa wale wanaopenda programu fupi, chuo kimesajiliwa na VETA|NACTVET toka Mwaka 2019 chuo kinauwezo wa kupokea wanafunzi 540”

“Kwa Mwaka jana 2021 chuo kilitoa mafunzo kwa wahitimu wa fani mbalimbali kama ifuatavyo wahitimu wa udereva 97, umekanika 8, ushonaji 5, umeme 12, uungaji vyuma 2 pamoja na kozi ya Kompyuta wahitumu 14 ambapo jumla yao ni 138”.

“Historia toka Mwaka 2018 chuo kimefundisha wanafunzi 498 wavulana wakiwa 400 na wasichana 98, kwa muda wote chuo kimepiga hatua kubwa kujenga (Erection) na ukarabati (Renovation) majengo ya bweni la wavulana na madarasa na karakana ya jengo la ufundi umeme, kujenga choo na tenki”.amesema mkuu wa chuo Kisanko

Baadhi ya wanafunzi wahitimu katika chuo hicho cha ufundi stadi Matanda VTC wemeahidi kufanya kazi kwa bidii ili kuendana na kasi ya mabadiliko ya teknolojia kwenye fani zao.

Wanafunzi wanaohitimu mafunzo ya ufundi katika fani mbalimbali kwenye chuo cha Matanda Vocational Training Centre ni pamoja na John Thomas Matemu, Ladslaus Silvest Tarimo, Mussa Ngasa Kasemele, Paskazia Ezekia Mashiku, Pius Godwin Rwengasira, Razalo Emmanuel Dotto, Brayan Patrick Okumu, Mathew Sylivester Mashalla. Norbert Elias Gabriel pamoja na Augustino John Manyenye.

 

 

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga mheshimiwa Elias Ramadhan Masumbuko akizungumza kwenye mahafali hayo

 

 

 mkuu wa chuo cha ufundi stadi Matanda Vocational Training Centre (VTC) Bwana Joaster Thomas Kisanko akisoma taarifa ya chuo

Wahitimu wakiwa katika mahafali yao








































































 

Post a Comment

Previous Post Next Post