Na Mapuli Misalaba, Shinyanga
Jeshi la polisi Mkoa wa Shinyanga linamshikilia mtu
mmoja kwa tuhuma za mauaji ya Mzee mmoja anayefahamika kwa jina la Raphael
Bundala mwenye umri wa Miaka 75 mkazi wa kijiji cha Kituli kata ya Tinde Halmashauri
ya Wilaya ya Shinyanga.
Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo Jumapili
majira ya saa tatu usiku huko katika
kitongoji cha Mwansami kijiji cha Kituli ambapo marehemu ameuawa kwa kukatwa na
Panga sehemu mbalimbali za mwili wake.
Misalaba Blog imezungumza na Kamanda wa jeshi la
Polisi Mkoa wa Shinyanga kamishna msaidizi wa Polisi Janeth Magomi ambaye
amekili kutokea kwa tukio hilo na kwamba tayari jeshi la polisi limemshikilia
mtuhumiwa mmoja kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria kuchukuliwa.
“Kwanza
ni mgogoro wa ardha mzee aliyeuawa huyu alikuwa anaugomvi wa muda mrefu na mototo
wa mdogo wake kijana wa kiume mzee huyu alikuwa akidai kuwa hilo shamba nila
marehemu mama yake na huyu kijana naye alikuwa akidai kuwa hilo shamba alipewa
na bibi yake kwahiyo mgogoro ulikuwa niwa muda mrefu”.
“Lakini
usiku huo zilifanyika juhudi huyo mtuhumiwa tayari tumeshamkamata ambaye
alikuwa na mgogoro wa ardhi”.amesema Kamanda Magomi
Aidha kamanda Magomi ametumia nafasi hiyo kuendelea
kutoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Shinyanga kuacha mara moja migogoro ya ardhi
huku akisema jeshi hilo limejipanga kupambana na wahalifu.
“Natoa
wito kwa wananchi wa Mkoa wa Shinyanga kuacha mara moja migogoro ya namna hii
kwa sababu tunakoelekea kwenye mvua
ndiyo hii migogoro inazidi lakini wito nikuacha mara moja na kufahamu kuwa
hakuna mtu ambaye huko juu ya sheria”.
“Na
sisi jeshi la polisi tumejipanga kunakikosi kazi ambacho kinafuatilia hawa
wakataji mapanga na tunamafanikio tu mazuri ambayo tunauhakika tutayakomesha
haya matukio”.amesema Kamanda Magomi
Kwa upande wake
Mwenyekiti wa kijiji hicho cha Kituli Bwana Ezekiel Shija ameeleza kuwa watu watatu wasiofahamika majina
walifika katika familia hiyo usiku baada ya hapo walianza kumshambulia Mzee
Raphael Bundala kwa kumkata panga na kupelekea kifo chake.
“Walikuja
mabwana watatu huo usiku mzee alikuwa ndani wale watoto walikuwa bado wapo nje
wanachema ni wajukuu wa marehemu baada ya kufika wale watu walimuulizia yule
mzee watoto walimwita akawa ametoka nje akawaambia karibuni sasa wale watu
wakamwambia sisi ni maaskari tunataka tufanye upelelezi waambie hawa watoto
waende ndani tuzungumze kweli mzee aliwaambia watoto wakaingia ndani”.
“Mzee
akashtuka naye baada ya kuona dalili siyo nzuri akataka kuingia ndani mmoja
akamzuia akatoa panga na kuanza mumkata yule mzee akamkata sehemu ya tumbo
upande wa kulia karibu na ubavu baadaye akamrudia tena nyingine akamkata
shingoni mzee akaanguka pale pale huku wale watoto wakiwa wanachungulia
dirishani”.ameeleza Mwenyekiti wa kijiji Bwana
Shija
Marehemu mzee Raphael Bundala alikuwa akiishi kwake
na familia yenye watoto sita (6) na kwamba mazishi yatafanyika leo majira ya
saa kumi jioni katika kitongoji cha Mwansami kijiji cha Kituli kata ya Tinde
mkoani Shinyanga.
Post a Comment