" ASKOFU BUGOTA AWAKUMBUSHA WAKRISTO KUTUMIA KARAMA ZAO KUACHA ALAMA KATIKA JAMII

ASKOFU BUGOTA AWAKUMBUSHA WAKRISTO KUTUMIA KARAMA ZAO KUACHA ALAMA KATIKA JAMII

Na Mapuli Misalaba, Shinyanga

Askofu wa kanisa la Africa Inland Church Tanzania AICT Dayosisi ya Shinyanga Zakayo Bugota amewakumbusha wakristo wajibu wa kutumia karama mbalimbali kuchochea maendeleo na ustawi wa kanisa na jamii ili kutimiza mapenzi ya Mungu.

Amesema kila mmoja kwa nafasi yake amebarikiwa karama ya aina yake ikiwemo taaluma, vipaji na maarifa hivyo ni vyema kutumia nafasi hiyo kutengeneza alama itakayodumu kizazi hadi kizazi.

Askofu Bugota ameyasema hayo leo Januari 15,2023 wakati akihubiri katika ibada ya Jumapili kwenye kanisa la AICT Kambarage mjini Shinyanga ambapo amesisitiza wakristo kutumia utume wao kwa lengo la kuchochea maendeleo na ustawi wa kanisa na kuwanufaisha wengine kama ishara ya kutii mapenzi ya Mwenyezi Mungu.

Amesema wakristo wanapaswa kutumika na kuacha alama zenye kumbukumbu za kimungu ambazo ni matokeo chanya katika jamii na Taifa kwa ujumla.

Askofu Bugota ambaye pia ni makamu mkuu wa Askofu kanisa la AICT amewasisitiza waumini wa kanisa hilo kuishi maisha yanayompendeza Mungu ili waweza kubarikiwa siku hadi siku.

Misalaba Blog imezungumza na baadhi ya waumini wa kanisa hilo ambao wamempongeza askogu Bugota kwa mahubiri hayo huku wakiwaomba wakristo wengine kutumia vipaji vyao kuleta matokeo chanya katika jamii.

waumini hao pia  wameahidi kuendelea kuzingatia mafundisho yanayotolewa na viongozi wa kanisa hilo ikiwa ni pamoja na kujitoa zaidi kumtumikia Mungu ili waweze kubarikiwa kizazi hadi kizazi.

Ibada ya jumapili katika kanisa la AICT Kambarage  imehudhuriwa na waumini,viongozi mbalimbali wa serikali na viongozi wa dini ndani na nje ya nchi wakiwemo wageni kutoka Nchini Kenya.Askofu wa kanisa la Africa Inland Church Tanzania AICT Dayosisi ya Shinyanga Zakayo Bugota akihubiri katika ibada ya leo kwenye kanisa la AICT Kambarage mjini Shinyanga.Ibada ikiendelea leo Jumapili Januari 15,2023 katika kanisa la AICT Kambarage mjini Shinyanga.

Post a Comment

Previous Post Next Post