Mwenyekiti wa Chama cha
Demokrasia na Maendeleo Chadema Bwana Emmanuel Ntobi amesema Chama hicho
kitaanza Mikutano ya hadhara
Mwezi Februari Mwaka huu ambapo uzinduzi
wake utafanyika katika Manispaa ya Shinyanga
Amesema uzinduzi
huo utatanguliwa na uzinduzi wa kitaifa
utakaofanyika kanda ya Victoria katika viwanja vya furahisha jijini
Mwanza ambapo mgeni rasmi atakuwa
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Bwana Freeman Mbowe.
Amefafanua zaidi kuwa
uzinduzi mwingine wa kanda ya Serengeti inayojumuisha Mikoa ya Shinyanga, Simiyu na Mara utafanyika katika Musoma Mkoani Mara.
“Mkoa
wa Shinyanga tumejipanga kuanza mikutano yetu ya hadhara Mwezi wa pili tutaanza
kuzindua katika Manispaa hii ya Shinyanga badae Kahama na majimbo mengine Ushetu,
Msalala, Solwa na Kishapu kwa sasa hivi tunasubiri kwanza ufanyike uzinduzi wa
Kitaifa ambapo utafanyika katika viwanja vya Furahisha jijini Mwanza ambapo
Mwenyekiti wa chama Freeman Mbowe ndiyo mgeni rasmi lakini pia tutaenda
kuzindua katika kanda yetu ya Serengeti kwa mikoa ya Shinyanga, Mara na
Simiyu ambapo uzinduzi utafanyika Mkoa wa Mara Musoma mjini katika viwanja vya
shule ya Kindwa na mkutano utaanza asubuhi saa mbili hadi saa kumi na mbili
jioni”.amesema Mwenyekiti Ntobi
Amesema CHADEMA
itafanya Mikutano yake kwa kuzingatia katiba na sheria za Nchi, kuuza sera
,kutumia majukwaa kidemokrasia kueleza sera mbadala,na ajenda zinazolenga
kuwasilisha hoja za kusaidia Wananchi.
Ntobi amewaomba
Wananchi wa Mkoa wa Shinyanga kufika kwenye mikutano hiyo ama kufuatilia kupitia
vyombo vya habari na mitandao ya kijamii,ili kuwasikiliza viongozi wa chama
hicho wakielezea sera na ajenda muhimu zinazolenga kuishinikiza serikali
kuwakwamua wananchi kutoka kwenye hali ngumu ya Maisha.
Hatua hiyo ya CHADEMA ni utekelezaji wa tamko la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan ambaye amerusu Mikutano ya hadhara kwa vyama vya Siasa Nchini.
Post a Comment