Na Mapuli Misalaba, Shinyanga
Mdau wa maendeleo wa Mkoa wa Shinyanga Caroline
Zacharia Mpemba jina maarufu Toffee up town ametoa msaada wa vitu mbalimbali
pamoja na kusherehekea na watoto wenye uhitaji katika shule inayomilikiwa na
shirika la Agape Mkoa wa Shinyanga.
Hafla hiyo imefanyika Jumamosi Januari 21,2023 katika
ukumbi wa Mazingira Center mjini Shinyanga ikiwa ni sehemu ya maadhimisho
kumbukizi ya siku ya kuzaliwa kwake Caroline Zacharia Mpemba almaarufu Toffee
up town.
Akizungumza katika hafla hiyo Toffee up town amesema
ni muhimu jamii kuonyesha upendo kwa watu wenye uhitaji na kwamba lengo la kutoa msaada huo ni
kupunguza changamoto zinazowakabili wanafunzi wanaomilikiwa na shirika la Agape.
Toffee up town pamoja na mambo mengine ametamka
rasmi kuwa ameamua kujitolea kuwa balozi wa shirika la Agape ambapo amesema
ataendelea kushirikiana nao ili kupunguza changamoto zilizopo na kwamba
wanafunzi hao waweze kufikia malengo yao.
"Mimi Caroline Mpemba Jina la Maarufu (Toffee Up Town) Nimefanya Jambo hili kama Mwanamke Mwenye Ushawishi Mkoa wa Shinyanga (Best Female Public Infruencer ) nilipata Tuzo Kupitia Taasisi ya HolySmile Mwaka 2021/2022. Hivyo nimefanya Jambo la Kijamii ili Kurudisha Shukurani kwa Jamii na Tukio hili ni Endelevu nitaendelea kufanya kwenye Jamii katika makundi mbalimbali ya wahitaji".
‘‘Nimeamua
kufanya hivi ili kutangaza upendo mjue kwamba kuna watoto wa Agape wapo
wanahitaji faraja zetu tuwatie moyo tuwafuata mara kwa mara huko kituoni kwao
na kwa kuwapelekea mahitaji, nawapenda sana watoto wangu na nimeamua kujitolea
kuwa balozi wenu kila kukicha nitawapambania mimi kama mama kama mlezi na kama
mdau wa maendeleo kwa leo nimewaandalia chakula tule pamoja na hili zoezi
litakuwa endelevu siyo kwamba nitaishia leo tu’’.amesema
Toffee up town
‘‘Nawashukuru sana viongozi wangu wa chama na
serikali pamoja na wadau mbalimbali kwa kunitia moyo na kunisapoti kwa hali na
mali katika shughuli yangu ya kusaidia watoto wenye uhitaji’’.amesema
Toffee up town
Kwa upande wake Mkurugenzi wa shirika la Agape Mkoa
wa Shinyanga John Myola amempongeza Toffee up town kwa majitoleo hayo huku
akieleza kuwa kituo hicho kinakabiliwa
na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa chakula, vifaa vya shule pamoja na
changamoto ya miundombinu.
‘‘Bado
tunauhitaji mkubwa kwa watoto wetu, hitaji la kwanza kabisa ni chakula lakini
hitaji lingine ni vifaa vya shule yaani matafutari kalamu na sale zingine za
shule pamoja na nguo zao binafsi wanahangaika sana lakini pia bado tunahitaji
miundominu majengo na vitu vingine vingi vinavyohitajika’’.amesema
Myula
‘‘Nawaomba
sana awe mama au baba na mtu yoyote mia tano kwetu ni hela kubwa sana tukinunua
chumvi itasaidia kwahiyo nawaomba kwa yoyote atakae guswa basi atuletee sisi
tutapokea aidha kipekee sana naomba nimshukuru Toffee up town kwa msaada wake
huu kwetu utapunguza changamoto tuliyonayo’’.amesema Myula
Naye mkurugenzi wa shirika la Fikra mpya akizungumza
kwa niamba ya mashirika Mkoa wa Shinyanga Leah Daud amewasihi wanafunzi
wanaosoma katika kituo cha Agape kusoma kwa bidii ili waweze kutimiza ndoto
zao.
Tofee up town ni mdau wa maendeleo wa Mkoa wa
Shinyanga alizaliwa Januari 18 ambaye husaidia serikali, chama pamoja na wadau
mbalimbali kufanikisha mambo kupitia njia mbalimbali ikiwemo mitandao ya kijamii.
Vitu vilivyotolewa leo kwa ajili ya watoto wenye
uhitaji katika kituo cha Agape ni pamoja
na Unga, Sukari, Sabuni, Mchele, Sabuni za unga, Juice maji, Biskuti pamoja na
fedha zikiwemo za viongozi na wadau mbalimbali walioguswa kuchangia.
Hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi wa serikali pamoja na wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa kikundi cha Shytown VIP na viongozi wa shirika la Lego Liquor Store.
Mdau wa maendeleo wa Mkoa wa Shinyanga Caroline Zacharia Mpemba jina maarufu Toffee up town akizungumza kwenye sherehe yake ya kumbukizi ya siku ya kuzaliwa.
Mkurugenzi wa shirika la Agape Mkoa wa Shinyanga John Myola akizungumza kwenye sherehe ya kumbukizi ya siku ya kuzaliwa Toffee up town.
mkurugenzi wa shirika la Fikra mpya akizungumza kwa niamba ya mashirika Mkoa wa Shinyanga Leah Daud akizungumza kwenye sherehe ya kumbukizi ya siku ya kuzaliwa Toffee up town.
Toffee up town akikabidhi msaada wake kwa mkurugenzi wa shirika la Agape Mkoa wa Shinyanga John Myola.
Zoezi la kukabidhi msaada wa vitu mbalimbali likiendelea katika ukumbi wa mazingira center.
Picha ya pamoja kabla ya kuanza zoezi la kula keki ambapo upande wa kushoto ni MC Mama Sabuni.
MC Zezema akizungumza kwenye sherehe ya kumbukizi ya siku ya kuzaliwa Toffee up town
Sherehe ya kumbukizi ya siku ya kuzaliwa kwa mdau wa maendeleo Mkoa wa Shinyanga Toffee up town ikiendelea katika ukumbi wa Mazingira center mjini Shinyang
Post a Comment