" WAISLAM WILAYA YA SHINYANGA WAACHE CHOKOCHOKO MWEZI MTUKUFU WA RAMADHAN- SHEKHE KATEGILE

WAISLAM WILAYA YA SHINYANGA WAACHE CHOKOCHOKO MWEZI MTUKUFU WA RAMADHAN- SHEKHE KATEGILE

 Na Mapuli Misalaba, Shinyanga

Wito umetolewa kwa waislam wote Wilaya ya Shinyanga kuishi matendo yanayompendeza Mwenyezi Mungu hasa katika kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhan.

Wito huo umetolewa leo na Shekhe wa Wilaya ya Shinyanga Sudi Kategile wakati akizungumza na Misalaba Blog ilipomtembelea ofisini kwake.

Kategile amewataka waislam kutumia kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhan kutenda matendo mema bila kubagua Dini wala kabila

Ametumia fursa hiyo kuwasisitiza waislam wote kutekeleza ibada ya funga katika kipindi hiki cha Mwezi  mtukufu wa Ramadhan.

Wakati huo huo Shekhe Kategile amewakumbusha waamini wa dini ya kiislam kuendelea kuomba Amani ya nchi ikiwa ni pamoja na kuombea viongozi wa serikali

Leo Waislam wameingia katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhan kwa siku 30, ndani ya wiki nne zijazo ambapo  mamilioni ya waislamu watajinyima kula na kunywa kuanzia mapema alfajiri hadi jioni.

 

Post a Comment

Previous Post Next Post