" MWENYEKITI WA CCM MKOA WA TABORA ALIYEFARIKI KUZIKWA KESHO

MWENYEKITI WA CCM MKOA WA TABORA ALIYEFARIKI KUZIKWA KESHO

 

Mjumbe wa Kamati kuu ya CCM, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tabora, Hassan Wakasuvi enzi za uhai wake.

Waziri mkuu Kassim Majaliwa anatarajiwa kuongoza viongozi wa ngazi mbalimbali wakiwemo wa vyama vya siasa, serikali na wananchi wakati wa mazishi ya aliyekuwa Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Tabora na mjumbe wa kamati kuu ya CCM Taifa Hassan Wakasuvi

Akitoa taarifa ya ratiba ya mazishi hayo katibu wa chama cha mapinduzi CCM Mkoa wa Tabora Elias Mpanda amesema kuwa mazishi hayo yatafanyika kesho katika kijiji cha Mabama ambako ndiko nyumbani kwa marehemu nje kidogo ya Manispaa ya Tabora.

Kwa mujibu wa mganga mfawidhi wa Hospitali ya rufaa ya Kitete Mkoani Tabora Dkt. Marco Waziri kifo cha ghafla cha Hassan Wakasuvi kilichotokea jana mchana kimetokana na shambulio la moyo.


Chama Cha Mapiduzi kikiongozwa na Mwenyekiti wake na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan , kimepokea kwa masikitiko makubwa na kutoa salamu za rambirambi na pole kwa ndugu, jamaa, marafiki na wanachama wote kufuatia kifo cha Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tabora Hayati. Hassan Wakasuvi.

Post a Comment

Previous Post Next Post