" MAGONJWA YASIYOYAKUAMBUKIZA YANATOKANA NA MTINDO AMBAO SIYO MZURI WA MAISHA - DKT. ZIZIMIZA

MAGONJWA YASIYOYAKUAMBUKIZA YANATOKANA NA MTINDO AMBAO SIYO MZURI WA MAISHA - DKT. ZIZIMIZA




Daktari wa magonjwa ya ndani katika Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Dkt. Mohamed Zizimiza akizungumza.

Na Mapuli Kitina Misalaba

Wakazi wa Mkoa wa Shinyanga wametakiwa kujitokeza kwenye kambi maalum ya upimaji na utoaji wa elimu ya magonjwa yasiyoyakuambukiza inayoendelea katika soko la Ngokolo mitumbani Manispaa ya Shinyanga.

Wito huo umetolewa na daktari wa magonjwa ya ndani katika Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Dkt. Mohamend Zizimiza ambaye amesema ni muhimu kila mtu kuwa na utamaduni wa kupima ili kufahamu hali ya afya yake.

Amesema magonjwa yasiyoyakuambukiza yanatokana na mtindo ambao siyo mzuri wa maisha ambapo amesema kuwa shinikizo la juu la damu ni  tatizo linaloongoza katika takwimu za wagonjwa wanaohudumiwa Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.

“Ukubwa wa tatizo la magonjwa yasiyoyakuambukiza kwa takwimu za Dunia ukienda katika magonjwa kumi (10) ambayo yanasababisha vifo Duniani ni magonjwa matatu yote ya mwanzo niyasiyoyakuambukiza kwahiyo tukija katika Hositali yetu katika Mkoa wetu kwa wagonjwa tunaopokea katika wodi zetu pamoja na wagonjwa wanaokuja Kriniki, wagonjwa wengi tunaopokea ni kutokana na magonjwa hayo yasiyoyakuambukiza ikiwamo pamoja na shinikizo la juu la damu, kisukari pamoja na uzito uliokisili”.

“Mara nyingi unapokuwa na magonjwa yasiyoyakuambukiza changamoto kubwa inatokana na mtindo usiokuwa mzuri wa maisha ambau unaweza kupelekea kupata uzito wenye kukisili umbao utasababisha kupata presha ambao ni shinikizo la juu la damu pamoja na kisukari lakini kwa takwimu za wagonjwa ambao tunawahudumia katika taasisi yetu tatizo la kwanza ambao linaongoza ni shinikizo la juu la damu ambalo pia changamoto yake tunayokutana nayo ni kuongezeka kwa wagonjwa ambao wanatatizo la kiharusi (Stroke)”.

“Wito wangu kwa wananchi ni kwamba magonjwa yasiyokuwa ya kuambukiza ni tishio si katika nchi yetu pekee yake ni katika Dunia nzima na si tishio tu katika afya lakini pia katika uchumi wan chi kwa sababu gharama za matibabu za magonjwa hayo ziko juu sana kwahiyo ninawasihi wananchi wa Mkoa wa Shinyanga na maeneo jirani kuhudhuria katika kambi hii ili kujua hali za afya zao lakini pia kwa wale ambao wamegundulika wawe na tabia za kuweza kufuatilia hali zao kwa kuhudhuria kriniki lakini pia kufuata maelekezo na ushauri wa wataalam wa afya”.amesema Dkt. Zizimiza

Amesema maratajia ya zoezi la upimaji na utoaji wa elimu ya magonjwa yasiyoyakuambukiza ni kuwafikia wananchi takribani mia tano.

Kwa upande wake afisa habari wa Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Bwana George Mganga amewasisitiza  wananchi kujitokeza kwa wingi ili kupata huduma bure za vipimo kwa magonjwa yasiyoyakuambukiza.

Amesema zoezi hilo linaendelea kutolewa bure ikiwa ni wiki maalum ya maadhimisho ya shinikizo la juu la damu Duniani, ambayo kauli mbiu yake inasema ‘Pima shinikizo la damu kwa usahihi, udhibiti, uishi muda mrefu’ na kwamba kilele chake ni Mei 17, 2024.

Baadhi ya wananchi walioshiriki zoezi hilo wameshukuru na kupongeza kwa huduma nzuri zinazotolewa katika kambi hiyo huku wakiomba huduma hizo ziweze kuendelea kutolewa katika maeneo karibu ya wananchi.

Kambi hiyo maalum ni kwa ajili ya upimaji bure wa magonjwa yasiyoyakuambukiza kama shinikizo la juu la damu (Presha), uzito, kisukari na elimu ya afya inayohusu magonjwa hayo pamoja na lishe.

‘Huduma katika kambi maalum Ngokolo mitumbani inatolewa kuanzia saa 2:00  asubuhi hadi saa 9:30 alasiri’

Afisa habari wa Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Bwana George Mganga akiwaomba wananchi kujitokeza kwenye kambi hiyo.

Afisa habari wa Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Bwana George Mganga akiwaomba wananchi kujitokeza kwenye kambi hiyo.

  

Mtoa huduma Jesse Samwel akimpima Mama mmoja wa wakazi wa Mkoa wa Shinyanga.



 

Post a Comment

Previous Post Next Post