" MWANAUME MMOJA AFARIKI AKIDAIWA KUNYWA GONGO KUPITA KIASI KATIKA MTAA WA CHAMAGUHA MANISPAA YA SHINYANGA

MWANAUME MMOJA AFARIKI AKIDAIWA KUNYWA GONGO KUPITA KIASI KATIKA MTAA WA CHAMAGUHA MANISPAA YA SHINYANGA

 

Na Mapuli Kitina Misalaba

Mwanaume mmoja anayeitwa Shaban Ally mwenye umri wa Miaka 40 mkazi wa mtaa wa Chamaguha Manispaa ya Shinyanga amefariki Dunia huku unywaji wa pombe ya kienyeji aina ya Gongo ukitajwa kuwa chanzo.

Tukio hilo limetolea Jumanne Mei 14,2024 na kwamba Misalaba Media imezungumza na Mwenyekiti wa mtaa wa Chamaguha Bwana Hussein Matamba ambaye ameeleza namna alivyopokea taarifa za tukio hilo kutoka kwa mke wa marehemu.

“Mimi nilipigiwa  simu kwamba kuna tukio hapa jirani kuna mtu amekufa basi nikaamua nifike pale nimeenda nikakuta kweli yule kijana anaitwa Shaban Ally amefariki alikuwa ni muuza matunda nikamuuliza mke kwamba ilikuwaje mpaka kufikia hatua ya kufa mke akasema siku ya Jumatatu marehemu aliondoka kwenda kwa ndugu zake aliondoka baada ya kumaliza kunywa chai lakini alikuja kurudi muda wa jioni akapitiliza kulala ndani akiwa anatoka jasho sana akamsemesha akaona haitikii akasema basi kwa kuwa amelala akapotezea akaendelea na shughuli zake tu akatoka maana wote huwa niwanywaji wa Pombe sana”.

“Alipokuja kurudi jioni akamuona yupo tu anajigeuza pale hakumjali nay eye akalala tu, amelala sasa kuamka asubuhi akamuona bado anahangaika hangaika akamuuliza kwamba nikukologee uji akakubali na hiyo sauti ya kukubali hakuzungumza tena yule mama aliendelea kukologa uje akamnywesha kama kikombe kimoja maana alimnywesha akiwa amelala wakati anaendelea kumnywesha uje akaona mwenzake analainika na kunyoka badae akajisaidia basi ikiwa umauti ndiyo umemfika kwa namna hiyo”. amesema Matamba

 

“Asilimia kubwa imeonekana Pombe ndiyo imesababisha maana huwa anabishara ya matunda asubuhi tu utamuona amelewa kwahiyo huwa anakunywa sana hizi Pombe za kienyeji na mimi huwa nawaambia sana waache hizo Pombe zao lakini vijana wa sasa hawaelewi”.amesema Matamba

Mwenyekiti huyo amesema baada ya kufika katika eneo la tukio amechukua hatua za kutoa taarifa hizo katika mamlaka mbalimbali ikiwemo jeshi la Polisi pamoja na ofisi ya mtendaji wa kata.

Misalaba Media imefanya juhudi za kumpata kaimu kamanda wa jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga haikufanikiwa.

 

 

 

 

 

 

Post a Comment

Previous Post Next Post