Ticker

6/recent/ticker-posts

MAMA NA WATOTO WAWILI WAFARIKI DUNIA BAADA YA KULA CHAKULA KINACHOSADIKIWA KUWA NA SUMU KISHAPU MKOANI SHINYANGA

Watu watatu wa familia moja Mama na watoto  wawili wamefariki Dunia wakati wakipatiwa matibabu katika kituo cha Afya cha Negezi tarafa ya Negezi Wilayani Kishapu  baada ya kula chakula kinachosadikiwa kuwa na sumu.

Taarifa hiyo imetolewa na kaimu kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga kamishina msaidizi wa polisi  Kenedy Mgani wakati akizungumza na Misalaba Media  ofisini kwake.

Amesema tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia jana Jumatatu Julai mosi, katika kitongoji cha Nyangalu, kijiji ca Mwajiginya A, Wilayani Kishapu  ambapo Mama na watoto hao wawili walikula chakula cha usiku lakini baadaye walianza kujisikia vibaya hali iliyowalazimu kuwahishwa kwenye kituo cha Afya  cha Negezi kwa ajili ya matibabu, lakini walifariki Dunia wakati wakipatiwa matibabu.

Ameeleza kuwa Uchunguzi zaidi unafanyika ili kubaini chanzo cha tatizo lililosababisha vifo vya wanafamilia hao watatu,na wengine wanne ambao wanaendelea na matibabu.

Post a Comment

0 Comments