" CCM SHINYANGA YASHUKURU WANANCHI KWA USHINDI WA KISHINDO KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024

CCM SHINYANGA YASHUKURU WANANCHI KWA USHINDI WA KISHINDO KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024

Na Mapuli Kitina Misalaba

Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Shinyanga wamewashukuru wananchi kwa kuwapa ushindi wa kishindo katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji, na Vitongoji uliofanyika hivi karibuni.

Kwa mujibu wa katibu Siasa, Uenezi na Mafunzo Mkoa wa Shinyanga Bwana Richard Raphael Masele, chama hicho kimefanikiwa kupata ushindi wa asilimia 100 katika mitaa 90 ya mkoa huo. Katika vijiji 506, CCM imeshinda vijiji 504, ikilingana na asilimia 96.6 ya ushindi. Aidha, chama hicho kimepata ushindi wa asilimia 99 katika vitongoji 2,703, kwa kushinda vitongoji 2,666.

Masele ameeleza kuwa ushindi huo utaimarisha juhudi za chama hicho katika kuwaletea wananchi maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

CCM imeahidi kuendelea kushirikiana na wananchi kuhakikisha kuwa ahadi zote zilizotolewa wakati wa kampeni zinatekelezwa kikamilifu kwa ustawi wa Mkoa wa Shinyanga.

 







Post a Comment

Previous Post Next Post