" BREAKING: MKURUGENZI WA MAWASILIANO CHADEMA AKAMATWA

BREAKING: MKURUGENZI WA MAWASILIANO CHADEMA AKAMATWA


Na: Belnardo Costantine, Misalaba Media

Jeshi la Polisi Nchini limethibitsha limetoa taarifa inayo eleza kumkamata  Bi. Brenda Rupia Jonas  mwanachama wa chama cha demekrasia na maendeleo "CHADEMA" mbaya pia  ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa  Chama hicho.

Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini DCP. David Misime imeeleza kuwa Bi. Rupia amekamatwa kwa ajili ya mahojiano kutokana na tuhuma zinazomkabili ikiwemo kutoa taarifa za uongo na za uchochezi.

Hata hivyo taarifa imeleza kuwa baada ya mahojiano taratibu nyingine kwa mujibu wa sheria za nchi zitafuata.


Sambamba na hilo CHADEMA ilitoa taarifa ya kuzuiwa kwa Mkurugenzi huyo ambaye alikuwa safarini kuingia Nchini Kenya kwaajili ya kikao kilicho kilichopangwa kabla ya kwenda Munich Ujerumani Kushiriki mafunzo ya kuhusu Demokrasia na Uchaguzi.



Post a Comment

Previous Post Next Post