Na Mapuli Kitina Misalaba
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Anamringi Macha, leo
Januari 25, 2025, amezindua rasmi maadhimisho ya Wiki ya Sheria, ambayo kilele
chake kitakuwa Februari 03, 2025.
Akizungumza katika uzinduzi huo, Jaji Mfawidhi wa Mahakama
Kuu Kanda ya Shinyanga Frank Habibu Mahimbali, amesema maadhimisho hayo yana
lengo la kuwaelimisha wananchi kuhusu namna Mahakama inavyofanyakazi chini ya
nguzo tatu za mpango mkakati wa Mahakama.
“Wataalam
wetu, wakiwemo mahakimu, majaji, wasajili, na maafisa wengine wa Mahakama,
wataeleza taratibu za kufungua mashauri Mahakamani, namna ya utoaji ushahidi,
ukazaji wa hukumu, na maamuzi yanayotolewa pia wananchi watapata nafasi ya
kutoa maoni na malalamiko yao,” amesema Jaji
Mahimbali.
Amebainisha kuwa huduma zote zinazotolewa kwenye
mabanda mbalimbali ni bure na amewahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi ili kufaidika
na fursa hiyo ambapo elimu itatolewa katika maeneo mengine ikiwemo shuleni, sokoni,
kwenye biashara mbalimbali, vituo vya bodaboda, na maeneo mengine ya kijamii.
Kauli mbiu ya maadhimisho hayo kwa mwaka huu ni: “Tanzania 2050: Nafasi ya
Taasisi Zinazosimamia Haki Madai katika Kufikia Malengo Makuu ya Dira ya Taifa
ya Maendeleo.”
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Anamringi Macha,
amepongeza juhudi za Mahakama katika kuwahudumia wananchi huku akiahidi
ushirikiano wa serikali.
“Sisi, kama mhimili wa utawala,
tutaendelea kushirikiana nanyi kwa ukaribu ili kuhakikisha haki inatamalaki haki
ikitamalaki, tutakuwa na taifa lenye amani, maendeleo, na ustawi wa wananchi,”
amesema RC Macha.
Kwa upande wake mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Wakili
Julius Mtatiro, akitoa salamu zake, amepongeza hatua za Mahakama katika kuleta
mapinduzi na maboresho ya huduma.
“Tunaendelea kuwakaribisha wananchi
kujionea huduma mbalimbali za kimahakama Wilaya yetu ni mahali salama, hivyo
nawahakikishia usalama wao watakapokuja kushiriki maadhimisho haya,”
amesema DC Mtatiro.
Baadhi ya wananchi waliopata huduma hizo wameeleza
kuridhishwa na huduma za haraka na bure zinazotolewa, huku wakitoa wito kwa
wengine kujitokeza ili kupata suluhisho la changamoto zao.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi
Macha, akizungumza wakati akizindua maadhimisho ya Wiki ya Sheria nchini kwa
Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Shinyanga leo Januari 25, 2025.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi
Macha, akizungumza wakati akizindua maadhimisho ya Wiki ya Sheria nchini kwa
Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Shinyanga leo Januari 25, 2025.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda
ya Shinyanga, Frank Mahimbali akizungumza kwenye uzinduzi wa maadhimisho ya Wiki ya Sheria
nchini kwa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Shinyanga leo Januari 25,
2025.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda
ya Shinyanga, Frank Mahimbali akizungumza kwenye uzinduzi wa maadhimisho ya Wiki ya Sheria
nchini kwa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Shinyanga leo Januari 25,
2025.
Mgeni rasmi katika uzinduzi wa maadhimisho ya Wiki ya Sheria nchini kwa
Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Shinyanga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi
Macha akitembelea mabanda mbalimbali.
Mgeni rasmi katika uzinduzi wa maadhimisho ya Wiki ya Sheria nchini kwa
Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Shinyanga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi
Macha akitembelea mabanda mbalimbali.
Mgeni rasmi katika uzinduzi wa maadhimisho ya Wiki ya Sheria nchini kwa
Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Shinyanga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi
Macha akitembelea mabanda mbalimbali.
Mgeni rasmi katika uzinduzi wa maadhimisho ya Wiki ya Sheria nchini kwa
Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Shinyanga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi
Macha akitembelea mabanda mbalimbali.
Mgeni rasmi katika uzinduzi wa maadhimisho ya Wiki ya Sheria nchini kwa
Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Shinyanga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi
Macha akitembelea mabanda mbalimbali.
Mgeni rasmi katika uzinduzi wa maadhimisho ya Wiki ya Sheria nchini kwa
Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Shinyanga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi
Macha akitembelea mabanda mbalimbali.
Post a Comment