

Mkuu wa Programu wa HelpAge Tanzania, Leonard Ndamgoba akiongoza mjadala wa makundi rika kwa wawakilishi kutoka kata za Idukilo, Mwamalasa na Mwamashele katika Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga.
Na Mapuli Kitina Misalaba
Shirika lisilo la
kiserikali la HelpAge Tanzania limeendesha mjadala wa makundi rika katika
Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga, likiwa na lengo la kukuza
usawa wa kijinsia, kutokomeza mila kandamizi, na kuimarisha afya ya uzazi hasa
kwa wanawake, wasichana na watu wenye ulemavu.
Tukio
hilo limefanyika ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Mradi wa Chaguo Langu, Haki Yangu, unaofadhiliwa na Serikali ya
Finland na kuratibiwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu (UNFPA)
kwa kushirikiana na wizara na taasisi mbalimbali.
Akizungumza
wakati wa majadiliano hayo, Leonard
Ndamgoba, Mkuu wa Programu wa HelpAge Tanzania, amesema shirika hilo
limeandaa mwongozo maalum wa majadiliano kati ya makundi ya wazee na vijana ili
kukabiliana na changamoto zinazoendelea kuikumba jamii.
"Tunashukuru
Serikali ya Finland kwa kufadhili mradi huu na UNFPA kwa usimamizi wa karibu.
Mwongozo huu unalenga kuvunja mila potofu kama ukeketaji, ndoa za utotoni na
ukatili wa kijinsia. Kupitia mijadala ya makundi rika, tunatengeneza jukwaa la
kuleta mabadiliko ya kweli kutoka kizazi kimoja kwenda kingine," amesema Ndamgoba.
Ameongeza
kuwa wawezeshaji waliopatiwa mafunzo wataendesha mijadala hiyo katika maeneo
mbalimbali ikiwemo mikutano ya hadhara, vikundi vya vijana na wazee, na hata
kwenye matukio ya kijamii kama misiba na harusi na kwamba wawezeshaji
waliobobea watawajengea uwezo wawezeshaji wapya ili kuendeleza juhudi hizo kwa
muda mrefu.
Majadiliano
ya makundi rika pia yanajikita katika kuziba pengo kati ya vizazi tofauti kwa
kuvunja mitazamo potofu ya kijinsia na kukabiliana na ukosefu wa usawa
uliojengeka kwa muda mrefu. Kwa kujenga mazingira salama ya mazungumzo,
wanawake na wasichana – hasa wenye ulemavu – wanapewa nafasi ya kudai haki zao
katika nyanja za elimu, uchumi, afya ya uzazi na ushiriki wa kijamii.
Mratibu
wa Mradi wa Chaguo Langu, Haki Yangu ambaye pia ni Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Ibrahim Sakulia, amewaomba wananchi
kutoa ushirikiano wa kutosha wakati wa hatua za utambuzi na utatuzi wa
changamoto mbalimbali za ukatili na mila kandamizi zinazozikabili jamii.
Amesema
ushirikiano wa wananchi ni msingi muhimu katika kufanikisha malengo ya mradi
huo unaotekelezwa na HelpAge kwa ufadhili wa Serikali ya Finland kwa
kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu (UNFPA).
“Lengo
letu ni kuifanya jamii ijitambue na ipate nafasi ya kujadili changamoto
zinazowakabili, zikiwemo ndoa za utotoni, ukeketaji na mila kandamizi.
Tunahitaji wananchi washiriki kikamilifu mijadala hii kwa sababu wao ndio
chachu ya mabadiliko tunayoyakusudia,” anasema Sakulia.
Katika
mafunzo hayo, wawakilishi wa makundi ya vijana na wazee kutoka kata hizo tatu
wamepewa mbinu za kuendesha midahalo ya makundi rika katika maeneo yao ili
kuchochea mijadala ya wazi juu ya ukatili wa kijinsia na namna ya kuukomesha
kwa njia ya majadiliano, usawa wa kijinsia, na heshima kwa haki za binadamu.
Kwa upande wake, Kaimu Mratibu wa Huduma za Mama na Mtoto
katika Hospitali ya Wilaya ya Kishapu, Hilda Ebunka, amesema hali ya
mimba za utotoni imeonesha kupungua ukilinganisha na miaka ya nyuma, jambo
linaloashiria mafanikio ya juhudi za pamoja kati ya serikali na mashirika ya
kiraia.
“Tulikuwa
tunapokea kesi nyingi za wasichana wadogo kupata ujauzito. Kwa sasa hali
imeanza kubadilika, ingawa bado tunahitaji kuendelea na elimu kwa jamii, hasa
maeneo ya vijijini,”
anasema Ebunka.
Afisa Ustawi wa Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Paul Lupolaso, amesema ofisi yake imekuwa ikipokea kesi
mbalimbali za ukatili, ambapo kubwa ni pamoja na ndoa za utotoni, ukatili wa kimwili, na unyanyasaji wa kiuchumi,
hasa kwa wanawake na watoto.
“Tunapokea
malalamiko kutoka familia mbalimbali. Ndoa za utotoni ni changamoto kubwa kwa
sababu huwakosesha watoto haki ya elimu, afya bora na maendeleo ya baadaye,” anasema Lupolaso.
Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto Wilaya ya Kishapu, Inspekta Rose
Mbwambo, amesema dawati hilo
limekuwa msaada mkubwa kwa wahanga wa ukatili wa kijinsia, huku akitoa rai kwa
jamii kushirikiana na jeshi la polisi kutoa taarifa mapema wanapobaini vitendo
vya kikatili ikiwa ni pamoja na kutoa ushahidi.
“Tunahitaji
jamii kushirikiana nasi kwa ukaribu. Wananchi wafahamu kuwa kazi ya dawati letu
ni kusaidia siyo kuadhibu. Tunapokea taarifa, tunachunguza na kuchukua hatua
kwa mujibu wa sheria,”
anasisitiza Inspekta Mbwambo.
Ametoa
wito kwa wazazi na walezi kuwafundisha watoto kuhusu haki zao, na kuhakikisha
wanawaweka salama dhidi ya ukatili wa aina yoyote ile.
Baadhi ya wananchi
kutoka kata za Idukilo, Mwamalasa na
Mwamashele wameeleza kuwa mafunzo hayo yamewapa maarifa mapya kuhusu
namna bora ya kupambana na ukatili wa kijinsia na kuendesha midahalo ya makundi
rika kwa lengo la kuhamasisha mabadiliko chanya kwenye jamii.
Wananchi
hao wamelishukuru shirika la HelpAge kwa kuwaleta pamoja na kuwapatia mafunzo hayo,
wakiahidi kuyatumia kikamilifu katika jamii zao ili kupunguza na hatimaye
kumaliza kabisa vitendo vya ukatili wa kijinsia.

Mkuu wa Programu wa HelpAge Tanzania, Leonard Ndamgoba akiongoza mjadala wa makundi rika kwa wawakilishi kutoka kata za Idukilo, Mwamalasa na Mwamashele katika Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga.

Mkuu wa Programu wa
HelpAge Tanzania, Leonard Ndamgoba
akiongoza mjadala wa makundi rika
kwa wawakilishi kutoka kata za Idukilo,
Mwamalasa na Mwamashele katika Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani
Shinyanga.
Mjadala wa makundi rika
kwa wawakilishi kutoka kata za Idukilo,
Mwamalasa na Mwamashele katika Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani
Shinyanga ukiendelea.

Mjadala wa makundi rika
kwa wawakilishi kutoka kata za Idukilo,
Mwamalasa na Mwamashele katika Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani
Shinyanga ukiendelea.


Mjadala wa makundi rika unaohusisha wawakilishi kutoka kata za Idukilo, Mwamalasa na Mwamashele katika Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga ukiendelea.

Mjadala wa makundi rika
unaohusisha wawakilishi kutoka kata za Idukilo, Mwamalasa na Mwamashele katika
Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga ukiendelea.
Mratibu wa Mradi wa Chaguo
Langu, Haki Yangu ambaye pia ni Afisa
Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Ibrahim Sakulia, akieleza hali ya ukatili wa kijinsia katika
Wilaya ya Kishapu.

Mjadala wa makundi rika
unaohusisha wawakilishi kutoka kata za Idukilo, Mwamalasa na Mwamashele katika
Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga ukiendelea.


Mratibu wa Mradi wa Chaguo
Langu, Haki Yangu ambaye pia ni Afisa
Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Ibrahim Sakulia, akizungumza.

Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto Wilaya ya Kishapu, Inspekta Rose
Mbwambo, akieleza hali ya
ukatili wa kijinsia na Ndoa za utotoni.

Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto Wilaya ya Kishapu, Inspekta Rose
Mbwambo, akieleza hali ya
ukatili wa kijinsia na Ndoa za utotoni.




Afisa Ustawi wa Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Paul Lupolaso, akizungumza kwenye mjadala huo wa makundi rika ambao
umeratibiwa na shirika la HelpAge Tanzania kupitia mradi wa Chaguo langu, Haki
yangu.
Afisa Ustawi wa Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Paul Lupolaso, akizungumza kwenye mjadala huo wa makundi rika ambao
umeratibiwa na shirika la HelpAge Tanzania kupitia mradi wa Chaguo langu, Haki
yangu.
Kaimu
Mratibu wa Huduma za Mama na Mtoto katika Hospitali ya Wilaya ya Kishapu Hilda
Ebunka, akizungumza kwenye mjadala huo wa makundi rika ambao umeratibiwa
na shirika la HelpAge Tanzania kupitia mradi wa Chaguo langu, Haki yangu.
Mjadala wa makundi rika ukiendelea katika Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu.









Mjadala wa makundi rika unaohusisha wawakilishi kutoka kata za Idukilo, Mwamalasa na Mwamashele katika Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga ukiendelea.

Mjadala wa makundi rika
kwa wawakilishi kutoka kata za Idukilo,
Mwamalasa na Mwamashele katika Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani
Shinyanga ukiendelea.

Mjadala wa makundi rika
kwa wawakilishi kutoka kata za Idukilo,
Mwamalasa na Mwamashele katika Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani
Shinyanga ukiendelea.

Mjadala wa makundi rika
kwa wawakilishi kutoka kata za Idukilo,
Mwamalasa na Mwamashele katika Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani
Shinyanga ukiendelea.







Post a Comment